Jumla ya washindi 62 mpaka sasa wamejishindia zawadi ya shilingi 50,000 kila mmoja na wateja wawili wakubwa wa wiki wamejishindia 1,000,000 kila mmoja katika droo ya kwanza na ya pili ya promosheni ya “SHINDA NA KABUMBU” iliyozinduliwa hivi karibuni ikiwa inawalenga wapenzi wa soka.

Washindi wa shilingi 1,000,000/-katika droo ya kwanza ni Salome Mayoba mkazi wa Kahama,na mshindi wa droo ya pili ni na Raymond Mwegoha mkazi wa Dar es Salaam ambapo washindi wa shilingi 50,000/- wametangazwa kuwa ni Hapifania Msack,Elick Mgecha,Jene Msangi,Pereus Ngambeki,Hassan Lugwisha, Wengine ni John Nkurlo,Makere Bairi,Jenro Ndimbudzi,Monica Mchilo,Ferida Nywage,Joseph Samwel,Yona Gilayo,Emil Mlutie,Batoromeo Nyerere,Peter Mbuya,Dismas Kimario,Vicent Mangesho,Sophia Segu,Omary Oswald,Zuberi Mwamba,Moses Mwambene,Wallace Ngalomba,Martin Dominick,Deusdediti Ziguye,Idd Joche,Swahab Said,Cleophace Gatahwa,Maneno Mwangosi,Peter Gabagambi,na Michael Kissla.

Promosheni hii ambayo itadumu kwa kipindi cha mwezi mmoja washindi wake wanapatikana kwa kujibu maswali mbalimbali kuhusiana na ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,Ligi kuu ya Uingereza,na masuala mengine mengi yanayohusiana na Kombe la Dunia na mengine mengi yanayohusiana na mchezo wa soka kwa ujumla.

Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amesema kila siku wapenzi wa soka au wateja 5 watajinyakulia shilingi 50,000 pia atakuwepo mshindi mmoja wa wiki atakaejinyakulia shilingi Milioni 1. Na droo ya mwisho katika promosheni hii atapatikana mshindi wa jumla atakayejinyakulia kitita cha shilingi Milioni 5 pesa taslimu. Ili kushiriki katika promosheni hii mpenzi wa soka au mteja yeyote wa mtandao huu anachopaswa kufanya ni kutuma neno SOKA kwenda namba 15725 na hapo mteja atakatwa kiasi cha shilingi 99 tu kwa kila meseji.

Amesema kila wiki washindi watakuwa wakitangazwa na kupigiwa simu moja kwa moja baada ya kufanyika droo za kila wiki na kutumiwa fedha zao kwa njia ya M pesa.

Vodacom imekuwa ikiandaa promosheni mbalimbali kwa wateja wake na moja ya promosheni ambayo imewafanya wateja wake maisha yao kuwa murua ni ile ya Timka na bodaboda na Vodacom milionea ambapo washindi waliweza kujishindia pikipiki na fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 100.
Humudini Abdulhussen Ofisa Mwandamizi wa Bodi ya Kusimamia Michezo ya Kubahatisha Tanzania (kushoto) akihakiki moja ya namba za simu anazoonyeshwa kwenye kompyuta mpakato na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (katikati) na Ofisa Masoko wa kampuni hiyo Prestin Lyatonga (kulia) wakati wa droo ya pili ya shindano la “Shinda na Kabumbu” inayowawezesha wadau wa soka na wateja wa kampuni hiyo kushiriki kwa kutuma neno SOKA kwenda namba 15725 na kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na soka. Zaidi ya wadau 60 wamejinyakulia pesa taslimu kupitia promosheni hii.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (katikati) akiongea kwa simu na Raymond Mwegoha mkazi wa Dar es Salaam aliyeibuka mshindi wa wiki na kujishindia kitita cha shilingi Milioni 1/= katika promosheni ya “SHINDA NA KABUMBU” inayoyawezesha wadau wa soka na wateja wa kampuni hiyo kushiriki kwa kutuma neno SOKA kwenda namba 15725 na kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na soka. Zaidi ya wadau 60 wamejinyakulia pesa taslimu kupitia promosheni hii. Wanaoshuhudia kushoto ni Ofisa Mwandamizi wa Bodi ya Kusimamia Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humudini Abdulhussen na Ofisa Masoko wa kampuni hiyo Prestin Lyatonga (kulia).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...