Wananchi wakiwa wamemzunguka Kakakuona aliyeonekana asubuhi majira ya saa moja maeneo ya Kigamboni Kisiwani Mtaa wa Chaboko ambapo kwa mujibu wa ripota na mpiga picha wetu Salma Bob Kassim, mnyama huyo aliwekewa Unga, ndizi, maji pamoja na pesa. 
Lakini akaishia kunywa maji tu kabla ya kukimbilia vichakani. Wananchi kwa mamia waliofurika kumuona Kakakuona huyo walisikika wakisema kuwa huenda huo ni utabiri kwamba huenda mvua zikawa nyingi msimu huu. 
Polisi walifika eneo la tukio na baada ya kuona hakuna uvunjifu wa amani wakatoa taarifa kwa maafisa wa Maliasili ambao walifika na kumtia mnyama huyo kwenye kiroba na kuondoka naye
 Kakakuona akijikunja baada ya umati wa watu kuzidi kuwa mkubwa 
Baadaye, huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha, Kakakuona huyo alielekea vichakani huku umati ukiendelea kumshangaa. Baadaye watumishi wa Maliasiali walifika na kumtia kwenye kiroba na kuondoka naye.
Picha na Salma Bob Kassim

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kuna ushahidi gani wa kisayansi wa kuunganisha kuonekana kwa kakakuona na kuwepo na mvua,baraka nk.au ndio jamii imekwama katika karne ya analog?

    ReplyDelete
  2. Lahaula ivi bado tupo ktk zama hizi....walau basi angetokea mmoja mwenye kukumbuka kadhia ya maisha kisha kuweka bendera au nembo ya ukawa na ccm.

    ReplyDelete
  3. Watu wanataka maji acheni kukariri kila siku kakakuona nawekewe maji,unga na fedha.....mungeweka nembo ya ukawa na ccm, vingine vyote vingejileta vyenyewe baada ya jinamizi kuwatoka....mkumbuke hivyo basi ndio nishawakumbusha huku nilipo kakakuona wapo ila sio dili.....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...