Pichani ni
maandalizi ya ujenzi wa mradi wa New Kawe City unaoendelea kwa kasi hivi sasa
katika eneo la Tanganyika packers,Kinondoni jijini Dar.Mradi huo unasimamiwa na Shirika la Nyumba la
Taifa (NHC).Camera ya Globu ya Jamii ilikatiza maeneo hayo jioni ya leo na
kujionea maandalizi makubwa ya ujenzi huo ambao wakazi wake watapata makazi
bora na ya kudumu kwa bei nafuu.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),Bwa.Nehemia Mchechu aliwahi kuzungumza kwenye moja ya jukwaa la uwekezaji wa sekta ya nyumba lililofanyika jijini Dar,na kueleza kuwa shirika hilo limedhamiria kuyabadilisha maeneo mengi ya jiji la Dar na mikoa mingine kuwa ya kisasa zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...