KIKOSI cha Usalama Barabarani
nchini kwa kushirikiana na Chama
cha Kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA)
limesema wataendelea kudhibiti upandishaji wa holela wa nauli za mikoani kuelekea katika sikukuu za kufunga
mwaka.
Akizungumza na waandishi wa
habari leo katika ukumbi wa idara ya habari Maelezo Kamanda wa Kikosi cha
Usalama Barabarani,Mohamed Mpinga
amesema watachukua hatua kali kwa mawakala wataopandisha nauli za mikoani.
Mpinga alisema kikosi cha usalama
barabarani kimejipanga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora usafiri kwa
bei zilizopangwa pamoja na kutoa onyo kwa madereva wanaoendesha mabasi na
magari kufuata sheria za usalama barabarani.
“Hatutavumilia mawakala na
madereva watakaokiuka sheria za usalama barabarani yote haya ni kutaka wananchi
wetu wasinyanyasike katika kipindi cha sikukuu siku zijazo sheria zimewekwa na
lazima watu wazifuate”alisema ,Mpinga.
Aidha alisema wananchi wanatakiwa
kutoa ushirikiano pale watapoona wanaopandisha nauli ili kuweza sheria ichukue
mkondo wake kukaa kimya kwa wananchi kunafanya jeshi kushindwa kuwabana watu
wanaofanya hivyo.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohamed R. Mpinga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu abiria kutoa taarifa kwenye mamlaka husika ili watetewa na fedha zao ziweze kurudishwa hata kama ni Tsh. 100/=.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...