Na Mwandishi Wetu

KOCHA wa mchezo wa masumbwi nchini,Rajabu Mhamila 'Super D' kwa kushirikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao wa kijamii wa whatsapp wamemkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea kwa ajili ya kuhamasisha mchezo wa masumwi nchini

vifaa hivyo vilivyotolewa na super D kwa kushilikiana na mdau mkubwa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mkumba ambaye ndie muhamasishaji mkubwa katika mtandao huo kwa ajili ya kusaidia mabondia

baada ya kukabidhiwa msaada huo bondia Mussa Chitepete wa Songea aliwashukuru wadau mbalimbali kwa kumpatia vifaa na kumpongeza kocha Super D kwa kuanzisha Kundi ambalo limekuwa muhimu sana kwake mpaka kupata vifaa hivyo.

nae mdau mkubwa wa masumbwi nchini Rajabu Mkamba amesema kwa kushirikiana na Super D wamefanya mambo mengi kwa ajili ya kuinua mchezo wa masumbwi nchini hivyo hawataishia hapo kwa kutoa sapoti kwa mabondia na wadau mbalimbali ili mchezo usonge mbele na wadhamini wajitokeze kusaidia ili vijana wawe na moyo wa kucheza mchezo wa masumbwi.
Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini,Rajabu Mhamila 'Super D' (katikati) akimkabidhi vifaa bondia Mussa Chitepete wa Songea vilivyotolewa nae kwa kushirikiana na marafiki zake wa kwenye mtandao. wengine kutoka kulia ni Kiliani Shayo na Rajabu Mkamba ambaye ni mdau mkubwa wa kuhamasisha kusaidia mchezo wa masumbwi na kushoto ni rafiki wa Bondia huyo. Picha na SUPER D BOXING 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...