Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia  wakazi wa KIMARA na TABATA; Miji ya Kibaha na Mlandizi mkoani Pwani  kuwa, Mtambo wa kuzalisha Maji wa Ruvu Juu umepata hitilafu kuanza siku ya Jumatano ya tarehe 03.12.2014 baada ya kuharibika kwa pampu moja ya kusukuma Maji (Pre-lift pump). 

Hali hii imelazimisha kupungua kwa uzalishaji Maji. 

Mafundi wa DAWASCO wanaendelea na matengenezo na kuhakikisha Pampu hii inafanya kazi na Huduma ya  Maji itarejea katika hali ya kawaida ifikapo siku ya Jumapili tarehe 07/12/2014
Wakazi wa maeneo yafuatayo wataathirika; MLANDIZI, KIBAHA, KIBAMBA, MBEZI, KIMARA, UBUNGO, MSEWE, KIBANGU, RIVERSIDE, BARABARA YA MANDELA, TABATA, NA SEGEREA.

PIGA SIMU KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA NAMBA 022- 2194800/ 0659-574012
DAWASCO INAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU AMBAO NI WA DHARULA.

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU
“DAWASCO TUTAKUFIKIA”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...