Baraza la Michezo la Taifa (BMT) chini ya udhamini wa taasisi ya UK Sports - Internationa Inspiration iliandaa mafunzo uhamasishaji wa michezo kwa vijana na watoto. Mafunzo hayo yaliyofanyika katika uwanja wa taifa yaliwakutanisha pamoja makatibu tawala pamoja na maafisa michezo toka katika wilaya zote nchini. Mafunzo hayo pia yalifanyika ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa Mwaka wa wa baraza la Michezo Tanzania uliofanyika katika uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Sihaba Mkinga, wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Makatibu Wakuu na Wenyeviti wa Kamati za Michezo za Mikoa Tanzania, uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. (picha kwa hisani ya Hivi Sasa Blog).
Baada ya mafunzo hayo, sherehe  rasmi ya uzinduzi wa kampeni ya Inspire Tanzania ilifanyika tarehe 20 September, 2014 katika uwanja wa taifa. Sherehe hiyo ilitanguliwa na mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) ambayo yaliratibiwa na klabu ya michezo ya Biafra pamoja na vilabu vingine vya jogging katika mkoa wa Dar es Salaam ambavyo Temeke Jogging, Faita, Jogging, Kopa Jogging, n.k.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...