Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli
kulia akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea, Chung Il kuhusiana
na mambo mbalimbali kuhusu sekta ya Ujenzi pamoja na mchakato
wa Ujenzi wa Daraja jipya litakalopita baharini pembezoni mwa daraja
la Selander.Daraja hilo litakuwa na urefu wa kilomita 7.2 na uwezo wa
kupitisha magari zaidi ya 61,000 kwa siku. Ujenzi wa Daraja hilo utaanza
muda wowote kuanzia sasa. Daraja hilo litakuwa na njia nne za magari
pamoja service road njia za waenda kwa miguu kila upande.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli
kulia akiagana na Balozi wa Jamhuri ya Korea Chung Il mara baada ya
kufanya mazungumzo ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana
jambo na Balozi huyo wa Jamhuri ya Korea Chung Il pamoja na Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe na Mkurugenzi wa Barabara
Eng. Ven Ndyamukama. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-
Wizara ya Ujenzi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...