Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea, Chung Il kuhusiana na mambo mbalimbali kuhusu sekta ya Ujenzi pamoja na mchakato wa Ujenzi wa Daraja jipya litakalopita baharini pembezoni mwa daraja la Selander.Daraja hilo litakuwa na urefu wa kilomita 7.2 na uwezo wa kupitisha magari zaidi ya 61,000 kwa siku. Ujenzi wa Daraja hilo utaanza muda wowote kuanzia sasa. Daraja hilo litakuwa na njia nne za magari pamoja service road njia za waenda kwa miguu kila upande.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akiagana na Balozi wa Jamhuri ya Korea Chung Il mara baada ya kufanya mazungumzo ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Balozi huyo wa Jamhuri ya Korea Chung Il pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe na Mkurugenzi wa Barabara Eng. Ven Ndyamukama. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Wizara ya Ujenzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...