Na Genofeva Matemu – Maelezo, Mbeya

Vijana wa Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Mbeya Vijijini wametakiwa kutokuwa na tafsiri hasi kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kuwa ni takrima inayotolewa na serikali kwa vijana hivyo kuchezea fedha hizo na kushindwa kurejesha mkopo watakaouomba kupitia mfuko huo.

Hayo yamesemwa na Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa wakati wa semina iliyotolewa kwa Vijana wa Mbeya Vijijini kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, Stadi za Maisha, Ujuzi na Ujasiriamali jana Mkoani Mbeya.

Bibi Riwa amesema kuwa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana unahudumia vijana wote nchini bila kuangalia itikadi za kisiasa ukiwa na lengo la kuwakomboa vijana na kuinua vipaji vya vijana nchi nzima.

“Vijana ni taifa la leo na kesho likiwezeshwa taifa zima limewezeshwa, Wizara yenye dhamana na Vijana inalenga kuwafikia vijana wote nchini bila kuangalia itikadi za kisiasa kwani vijana wote ni wetu na tunatamani kuona vijana wanajiendeleza kufikia ndoto walizonazo” amesema Bibi Riwa.

Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbeya Vijijini Bibi Upendo Sanga amesema kuwa ni bahati ya pekee kutembelewa na ugeni kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivyo kuwaomba vijana wa Wilaya yake kuzingatia elimu watakayoipata na kusambaza elimu hiyo kwa vijana wengine wa Wilaya yake ambao hawakuweza kufika katika semina hiyo.

Bibi Sanga ameiomba Wizara yenye dhamana na Vijana kuendeleza programu ya kuwaelimisha vijana mara kwa mara na kuwahamasisha vijana kujiunga katika vikundi kwani ni raisi kusaidia vijana wakiwa katika vikundi kuliko kumsaidia kijana mmojammoja.

Akichangia wakati wa semina hiyo kijana Evans Bembeja kutoka Shirika la Efao linalojishughulisha na kilimo cha mbogamboga amesema kuwa vijana wengi hawaangalii mbele wamekua kwenye mwamko wa kisiasa wakiamini kuwa siasa ndio sehemu ya kupata pesa za haraka hivyo kuachana na fursa nyingine kama vile kilimo na ufugaji.
Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini Bibi Upendo Sanga akifungu semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo jana katika Mkoa wa Mbeya. Waliokaa katikati ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa na kulia ni Afisa Vijana kutoka Wizara hiyo Bi. Amina Sanga.
Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akiwaelimisha vijana wa Wilaya ya Mbeya Vijijini kuhusu mwongozo unaosimamia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri hiyo Mkoa wa Mbeya.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...