Na Andrew Chale
Bendi ya taarab ya 'Gusa Gusa Min Band,'  inatarajiwa kurindima kila Jumapili katika usiku wa Old is Gold Taarab ndani ya ukumbi wa Safari Carnival, Mikochezni B, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa waandaji wa usiku huo, Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin, kila Jumapili bendi hiyo ya Gusa Gusa itakuwa ikitoa burudani ya kipekee kwa  nyimbo za taarab zikiwemo za zamani na zile za kisasa.
"Kila jumapili  kwa kiingilio cha sh 5,000 tu. Wapenzi wa muziki wa mwambao  watafurahia bendi ya Gusa Gusa ndani ya Usiku wa Old is Gold katika ukumbi wa Safari Carnival” alisema Asia Idarous.
Asia Idarous amewasihi wapenzi na wadau kujitokeza kwa wingi kushuhudia bendi hiyo pamoja na kukumbushana yale ya zamani na kubadilishana mawazo.
Mdau huyo Asia Idarous aliongeza kuwa, usiku huo uliodhaminiwa na  Safari Carnival, Fabak fashions, Clouds fm, Gone Media, Maji Poa, Michuzi Media Group na wengineo, utakuwa wa aina yake kwa kila atakayefika ukumbini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...