Watu wenye uhitaji wa msaada wa sheria sasa wanaweza kupata huduma hiyo kwa kuingia mtandaoni baada ya wakili mmoja Jijini Dar es Salaam kuanza kutoa huduma hiyo.

Wakili Emmanuel Augustino ameanza kuwafikia wahitaji wa msaada wa sheria kwa kutumia blog yake ya wakiliwangu.blogspot.com.

"Kupitia blog hii, tunatoa ushauri wa kisheria wa mambo yanayohusu mirathi, ununuzi au uuzaji wa ardhi, kesi za jinai na madai, kuanzisha kampuni na mambo mengine tofauti ya kisheria," alisema Wakili Augustino.

Wakili Augustino anasema kuwa wazo la kutoa msaada wa kisheria kwa njia ya mtandao lilimjia baada ya kuhudhuria mkutano mkuu wa chama cha wanasheria wa Afrika Mashariki kilichofanyika Kigali, Rwanda mwaka huu.

"Kule Kigali, kulikuwa na mjadala kuhusu matumizi ya teknologia kuwafikia wateja. Wanasheria maarufu walisema kuwa ni namna bora ya kuwafikia watu, badala ya utaratibu tuliouzowea wa kufuatwa ofisini," alisema.

"blog ya wakiliwangu.blogspot.com ni kwa ajili ya watu wasio na uwezo. Tunachokifanya ni kutoa ushauri na pia msaada wa kuandika nyalaka tofauti zinazohitajika kukamilisha mchakato wa kisheria kama kuandika wosia, kuandika mikataba, n.k. Tunatoa msaada kwa njia ya simu, e­mail," aliongeza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...