Na Bashir Yakub
Katika makala iliyopita nilisema kuwa vijana wengi wajasiriamali wanaofungua biashara za makampuni wanao uwezo mkubwa wa kufika mbali isipokuwa tatizo lao ni taarifa za mambo mbalimbali kuhusu uendeshaji wa kampuni hizo.
Mambo ya uendeshaji wa kampuni ni mepesi sana na yanawezwa na mtu yeyote isiopokuwa tatizo ni taarifa na elimu ya namna ya uendeshaji kisheria ili kampuni ionekane ni kampuni. Nilieleza namna kampuni inavyolipa kodi na taratibu za kikodi za kampuni.
Leo tuangalie kipengele kingine cha uendeshaji wa kampuni ambacho ni namna ya kupata leseni ya biashara.
1. KAMPUNI ULIYOSAJILI HAIWEZI KUANZA KAZI BILA LESENI YA BIASHARA.
Wajasiriamali wengi wanaofungua kampuni wanajua kuwa ukishapata usajili wa kampuni basi unakuwa umemaliza kila kitu na unaweza kuanza biashara. Wazo hili si la kweli kwakuwa baada ya kampuni kuwa imepata usajili na unataka kuanza biashara ni lazima uwe na leseni ya biashara (business licence). Kwa maana hii kumbe mchakato wa kuanza biashara na kampuni hauishii kwenye kupata usajili wa kampuni. Cheti cha kuzaliwa kwa kampuni yako ( certificate of incorporation) ni tofauti na leseni ya biashara.Na ili biashara ya kampuni ianze kisheria lazima uwe navyo vyote viwili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...