Na   Bashir     Yakub

Katika  makala  iliyopita  nilisema  kuwa  vijana  wengi   wajasiriamali  wanaofungua   biashara  za  makampuni   wanao  uwezo  mkubwa   wa kufika mbali   isipokuwa  tatizo  lao  ni  taarifa za  mambo  mbalimbali   kuhusu uendeshaji  wa  kampuni   hizo. 

 Mambo  ya uendeshaji   wa  kampuni  ni  mepesi sana  na  yanawezwa   na  mtu  yeyote isiopokuwa   tatizo   ni   taarifa   na  elimu ya  namna  ya  uendeshaji  kisheria   ili   kampuni   ionekane  ni kampuni.  Nilieleza  namna   kampuni  inavyolipa kodi   na  taratibu  za   kikodi  za kampuni.

  Leo tuangalie  kipengele  kingine  cha  uendeshaji  wa kampuni  ambacho  ni namna  ya   kupata   leseni  ya   biashara.

1. KAMPUNI   ULIYOSAJILI   HAIWEZI   KUANZA   KAZI   BILA   LESENI    YA BIASHARA.

Wajasiriamali   wengi   wanaofungua kampuni   wanajua   kuwa   ukishapata usajili   wa   kampuni   basi    unakuwa umemaliza   kila   kitu   na   unaweza  kuanza   biashara.  Wazo  hili  si   la  kweli kwakuwa  baada  ya  kampuni  kuwa  imepata usajili  na    unataka   kuanza biashara   ni   lazima  uwe   na   leseni   ya biashara (business  licence).  Kwa   maana   hii   kumbe  mchakato   wa kuanza   biashara   na   kampuni   hauishii kwenye  kupata     usajili   wa   kampuni. Cheti  cha  kuzaliwa  kwa  kampuni  yako ( certificate  of  incorporation)  ni  tofauti na  leseni   ya   biashara.Na   ili  biashara  ya  kampuni  ianze  kisheria  lazima  uwe  navyo  vyote  viwili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...