Na Faustine Ruta, Bukoba
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Jamal Emil Malinzi wa pili kutoka (kushoto) akiongozana na Baadhi ya Viongozi wa Mpira hapa Nchini leo hii Mchana alipowasili katika Uwanja wa Kaitaba unaokarabatiwa kuwekwa Nyasi za Bandia. Bw. Jamal Emil Malinzi pia ndie Mwenyekiti wa chama cha mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA) alipowasili hapa Bukoba amezungumza na Viongozi wa Soka Mkoani hapa Kagera na baadae.
Rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi pia aliambatana na Viongozi mbalimbali hapo Uwanjani akiwemo Bw. Pelegrinius A. Rutayuga, Mjumbe wa kamati Tendaji ya KRFA , Mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF na Mshauri Mkuu wa Kiufundi TFF makao makuu, Katibu wa KRFA Salumu Umande Chama ambaye pia ni Kiongozi kamati ya Waamuzi Nchini.
Doron Mommsen(kushoto) akiongea na Rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi(kulia) leo wakati Rais huyo alipotembelea kujionea Ukarabati huo wa Uwanja wa Kaitaba ambao Utachukua Muda wa Miezi Mitatu. Meneja wa Mradi Bw. Doron Mommsen amemweleza Ndugu Jamal Malinzi kwamba Ukarabati unaendelea Vizuri na kinachoendelea kwa sasa ni kusawazisha Udongo katika Uwanja huo.
Meneja wa Mradi Bw. Doron Mommsen akionesha kile kinachoendelea atika Uwanja huo wa Kaitaba. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...