Hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Taifa kwa Wanawake inachezwa kesho (Januari 26 mwaka huu) na Januari 27 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam kwa mechi mbili kila siku.

Mechi ya kwanza ya robo fainali ya michuano hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Televisheni itaanza saa 9 alasiri kwa kuzikutanisha Mwanza na Kigoma. Robo fainali ya pili ambayo ni kati ya Tanga na Pwani itaanza saa 11 kamili jioni.

Ilala na Iringa watacheza robo fainali ya tatu Januari 27 mwaka huu kuanzia saa 9 kamili alasiri, na kufuatiwa na robo fainali ya mwisho saa 11 kamili jioni itakayozikutanisha Temeke na Mbeya.

Nusu fainali za michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Proin zitachezwa Januari 29 mwaka huu wakati Fainali itachezwa Februari Mosi mwaka huu kuanzia saa 10.15 jioni ambapo itatanguliwa na mechi ya kutafuta mshindi wa tatu (play off).

Timu zote zilizoingia hatua hiyo ya nane bora ya michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini zimefikia hosteli ya Msimbazi.

Wakati huo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika kesho (Januari 26 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...