MNAMO TAREHE 23, 24 NA 25 JANUARI 2015, SHIRIKA LA MAJI SAFI NA MAJITAKA DAR-ES-SALAAM (DAWASCO) ILIZIMA MTAMBO WA RUVU CHINI ILI KURUHUSU MKANDARASI KUUNGANISHA BOMBA JIPYA NA LA ZAMANI (CROSS –SECTION). HATA HIVYO BAADA YA KAZI KUKAMILIKA NGUVU YA MAJI ILISABABISHA KUYUMBISHA SEHEMU ILIYOUNGANISHWA AWALI.

HALI HII IMESABABISHA HUDUMA YA MAJI KUKOSEKANA KWENYE BAADHI YA MAENEO YA JIJI LA DAR ES SALAAM KUANZIA ALHAMISI 29/01/2015  
 KWASABABU HIYO MAENEO YAFUATAYO YAMEKOSA MAJI:

MJI WA BAGAMOYO, VIJIJI VYA MAPINGA, KEREGE NA MAPUNGA. BUNJU, BOKO, TEGETA, KUNDUCHI, SALASALA, JANGWANI, MBEZI BEACH NA KAWE.

MAENEO MENGINE NI MLALAKUWA, MWENGE, MIKOCHENI, MSASANI, SINZA, MANZESE, MABIBO, KIJITONYAMA, KINONDONI, OYSTERBAY, MAGOMENI, UPANGA, KARIAKOO, CITY CENTRE, ILALA, UBUNGO MAZIWA, KIGOGO, MBURAHATI, HOSPITALI YA RUFAA MUHIMBILI, BUGURUNI, CHANGOMBE NA KEKO.

MKANDARASI ANAENDELEA NA MATENGENEZO NA HUDUMA YA MAJI ITAREJEA TENA BAADA YA SAA 12 KUANZIA LEO.       
         
WANANCHI MNASHAURIWA KUHIFADHI MAJI NA KUYATUMIA KWA MATUMIZI YA LAZIMA.

DAWASCO INAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU
“DAWASCO TUTAKUFIKIA”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...