Na Anitha Jonas - MAELEZO.

SERIKALI imedhamiria kupunguza msongamano wa magari  ndani ya jiji la Dar es Salaam kwakujenga barabara sita zitakazo ambazo ujenzi wake utasimamiwa na TANROADS. Ujenzi huo unatarajiwa kugharimu sh. trilioni moja ambapo lengo barabara hizo ni  kupunguza adha ya msongamano wa magari  katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es saalam.

Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akiweka jiwe la msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara hizo. “Barabara hizi zinajenga kwa ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 100 na lengo kubwa la mradi huu ni kupunguza msongamano ndani ya jiji” alisema Magufuli.

Magufuli aliendelea kusema “Rai yangu kwa Watanzania  wote ikiwemo madereva wa magari yenye uzito mkubwa  kuacha kupita barabara zisizo stahimili uzito wa magari hayo na kuwaasa wananchi wa maeneo jirani waache  kugeuza  barabara hizo kuwa maduka au fremu za biashara”.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Said Mecky Sadick aliwaasa wananchi wa Dar es Salaam kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali na wakandarasi pale watakapoombwa wasogee  nje ya barabara ili kufanikisha ujenzi huo kwani barabara ni sehemu ya maendeleo na ni vyema kila mmoja kuwa mzalendo na kuacha itikadi za vyama .

“Nikiwa kama mdau mkubwa wa maendeleo ya jiji la Dar es Salaam nitahakikisha wakandarasi hawa wanamaliza kazi ya ujenzi huu  kwa wakati na nitakuwa nikiwafuatilia kwa karibu katika kuhakikisha  viwango  vinazingatiwa  ili barabara hizi ziweze kuwa mkombozi wa tatizo la msongamano katika jiji,” alisema Sadick.

Kwa upande wake Mtendaji  Mkuu Wakala wa Usimamizi wa Barabara (TANROADS) Mhandisi  Patrick Mfugale alizitaja barabara zinazotarajiwa kuanza kujengwa katika mradi wa kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam ni Ubungo Msewe hadi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye urefu wa kilomita 2.6, Ubungo Externo hadi Kilungule kilomita 3, Kigogo hadi Tabata Dampo kilomita 1.6.

Mfugale alisema kuwa barabara nyingine ni Kinyerezi hadi Kifuru kilomita 4 kwa awamu ya kwanza na badae ni Kifuru hadi Maramba Mawili kilomita 10, pamoja na Mbezi Mwisho hadi Goba Tangi Bovu ambayo ni kilomita 20.
Katika Ziara hiyo ya kuweka jiwe la msingi Waziri Magufuli aliambatana na watendaji na viongozi wa TANROADS, wabunge wa maeneo hayo, watendaji wa wizara.



                                  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...