Na Bashir Yakub
Nimeandika makala nyingi kuhusu namna  ya kisheria ya kuepuka  kununua nyumba/viwanja  vyenye  migogoro kwakuwa  migogoro ya vitu hivi inaumiza sana. Waliokutana na migogoro hii wanajua  vyema ninaongea nini. 
Katika mwendelezo wa kumuepusha mnunuzi  na janga hili, leo tena tuangalie taratibu za ununuzi wa nyumba/kiwanja cha  mirathi. Nataka ieleweke vyema kuwa taratibu za manunuzi ya nyumba/kiwanja  zinatofautiana. 
Tofauti kubwa  ni za kisheria hasa  namna ya uandishi wa mkataba  na nyaraka ambazo  zitaambatana na  mkataba huo. Eneo hili nalo naliongelea kwakuwa ni eneo ambalo kwa upande wake nalo limewaingiza wanunuzi wengi wa nyumba/viwanja katika migogoro  ambayo ingeweza kuepukwa mapema iwapo taarifa kama hizi pengine mnunuzi angezipata  mapema.  Kisheria si kweli kuwa kila aina ya mkataba  unaweza kut umika kununua kila aina ya nyumba. 
Mkataba huandaliwa kutegemea na mazingira ya kitu chenyewe. Nyumba/kiwanja ambacho wauzaji wake  ni wasimamizi wa mirathi ni tofauti na nyumba/kiwanja ambacho  muuzaji si msimamizi mirathi.  Tatizo  kubwa ambalo limewasumbua wengi mahakamani ni kununua nyumba/kiwanja  cha  mirathi  kwa  kutumia  utaratibu uleule  wa kununulia kiwanja/nyumba ya kawaida ambayo muuzaji wake ni mmiliki halisi  yaani si msimamizi wa mirathi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...