Na Bashir Yakub
Nimeandika makala nyingi kuhusu
namna ya kisheria ya kuepuka kununua nyumba/viwanja vyenye
migogoro kwakuwa migogoro ya vitu
hivi inaumiza sana. Waliokutana na migogoro hii wanajua vyema ninaongea nini.
Katika mwendelezo wa
kumuepusha mnunuzi na janga hili, leo tena
tuangalie taratibu za ununuzi wa nyumba/kiwanja cha mirathi. Nataka ieleweke vyema kuwa taratibu
za manunuzi ya nyumba/kiwanja zinatofautiana.
Tofauti kubwa ni za kisheria hasa namna ya uandishi wa mkataba na nyaraka ambazo zitaambatana na mkataba huo. Eneo hili nalo naliongelea
kwakuwa ni eneo ambalo kwa upande wake nalo limewaingiza wanunuzi wengi wa
nyumba/viwanja katika migogoro ambayo ingeweza
kuepukwa mapema iwapo taarifa kama hizi pengine mnunuzi angezipata mapema. Kisheria si kweli kuwa kila aina ya
mkataba unaweza kut umika kununua kila aina
ya nyumba.
Mkataba huandaliwa kutegemea na mazingira ya kitu chenyewe. Nyumba/kiwanja
ambacho wauzaji wake ni wasimamizi wa
mirathi ni tofauti na nyumba/kiwanja ambacho
muuzaji si msimamizi mirathi.
Tatizo kubwa ambalo limewasumbua
wengi mahakamani ni kununua nyumba/kiwanja
cha mirathi kwa
kutumia utaratibu uleule wa kununulia kiwanja/nyumba ya kawaida ambayo
muuzaji wake ni mmiliki halisi yaani si
msimamizi wa mirathi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...