Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(kushoto) na Mkuu wa kitengo cha mazingira wa manispaa hiyo Themi Luther(kulia) wakipitia michoro ya usanifu ya majengo kwenye makutano ya mitaa ya Aggrey na Indraghandi ambapo ujenzi huo haujafuata michoro, Alipotembelea na kupima uzio wa mabati unaowekwa na wakandarasi wengi bila kulipiwa vibali, Katika ukaguzi huo majengo mengi yamekiuka michoro ya ujenzi na amesimamisha ujenzi huo mara moja hapo jana.
Mkuu wa kitengo cha mazingira wa manispaa ya Ilala Themi Luther(katikati)akimpatia maelekezo .Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(kushoto) kuhusiana na usanifu wa jengo kwenye makutano ya mitaa ya Aggrey na Indraghandi ambapo ujenzi huo haujafuata michoro,Meya huyo alitembelea na kupima uzio wa mabati unaowekwa na wakandarasi wengi bila kulipiwa vibali, Katika ukaguzi huo majengo mengi yamekiuka michoro ya ujenzi na amesimamisha ujenzi huo mara moja hapo jana.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(katikati mwenye miwani) akitaka ufafanuzi wa michoro ya majengo kwa mmoja wa waandisi wanaojenga majengo yaliyopo katika makutano ya mitaa ya Aggrey na Indraghandi ambapo baadhi ya majengo hayo hayajafuata michoro sanifu,Meya huyo alitembelea na kupima uzio wa mabati unaowekwa na wakandarasi wengi bila kulipiwa vibali, Katika ukaguzi huo majengo mengi yamekiuka michoro ya ujenzi na amesimamisha ujenzi huo mara moja hapo jana.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(wapili toka kushoto) na Naibu wake Khery Kessy Mohamed(katikati)wakipima michoro ya usanifu ya jengo kwenye makutano ya mitaa ya Aggrey na Indraghandi ambapo ujenzi huo haujafuata michoro halali ya ujenzi,Walipotembelea na kupima uzio wa mabati unaowekwa na wakandarasi wengi bila kulipiwa vibali, Katika ukaguzi huo majengo mengi yamekiuka michoro ya ujenzi na amesimamisha ujenzi huo mara moja hapo jana.
Waandisi wanaojenga majengo yaliyopo katika makutano ya mitaa ya Aggrey na Indraghandi wakisisitizwa jambo na Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa(katikati mwenye miwani)wakati alipotembelea na kupima uzio wa mabati unaowekwa na wakandarasi wengi bila kulipiwa vibali na kukagua majengo mengi ambayo yamekiuka michoro ya ujenzi na amesimamisha ujenzi huo mara moja hapo jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Ankal,

    Indragadhi ndo mtaa gani katikati ya jiji letu la Dar-es-Salaam, Tanzania?

    Michuzi najua wewe ni motto wa mjini uliokulia jijini Dar-es-Salaam, makosa ya uandishi kama huu hatutegemei kabisa.

    Jina la mtaa ni Indira Gandhi, jina la Waziri Mkuu wa zamani wa nchi ya India.

    Mdau
    Mtoto wa Mjini

    ReplyDelete
  2. Kwa habari kama hizi, inapaswa wadau kutupatia angalau picha ya hili jengo ili na sisi tuweze kuiangalia.

    ReplyDelete
  3. i think mdau mjuaji michuzi ameeleweka anamaaisha nini na wewe tafuta blog yako uandike unavyojua wewe

    ReplyDelete
  4. mradi ulielewa ndiyo hiyo hiyo

    ReplyDelete
  5. Hongera sana slaa na mlete engineer akaguwe sslap ya kwanza mpaka. Nne pande zote nazo zimepinda,ujenzii wa jengo hili ni utata mtupu na ninaomba sana hili jengo lisimamishwe ikibidi lifunjwe msigoje mpakaa liwe kubwa halafu mshindwe kutolea mamuzi

    ReplyDelete
  6. Jengo hili linamilikiwa na mfanya biashara maarufuu na liko chini ya standard ambayo ma engineer wa jiji wasifungiye macho kwani hata Sisi tusiokwenda shule na akili yetu timamu Tunaona nakueelewa kama ujenzi ni mpovu na ukaguzi wa michoro na slap zilivyowekwa na kupinda ni ushahidi kamili

    ReplyDelete
  7. Meya ninakukumbusha lile jengo liloporomoka na kuua watu na bado halijavunjwa mpaka leo kwanza ni hatarishi na siku wahusika waliokalia kimya mpaka leo ndiyo watakuwa wafunguliwe mashataka

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...