Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya ya Mkuranga,Benjamini Majoya akipokea msaada uliotolewa na Kampuni ya Upendo Media Group,Benki ya Maendeleo na Fifa Flow Limited kwa Mteule Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani,Chediel Luiza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika viwanja vya Azania Front Jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
AFISA Elimu Sekondari,Wilaya ya Mkuranga Benjamini
Majoya amekishukuru Kituo cha Radio cha Upendo pamoja na gazeti la Upendo kwa kutoa
habari za Wilaya ya Mkuranga na kupata msaada wa madawati pamoja na sare
za shule kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu.
Majoya ametoa shukrani hizo wakati akikabidhiwa
madawati 40 na sare kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu iliyofanyika leo
katika viwanja vya Azania Front jijini Dar es Salaam.
Madawati na sare kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalumu zimetolewa na Benki ya Maendeleo ,Kampuni Fifa Flow Limited pamoja na
Kituo cha Radio Upendo pamoja gazeti la upendo.
Msaada huo umetokana na Kituo cha Radio Upendo
pamoja gazeti la upendo kwenda katika Wilaya ya Mkuranga kutafuta habari na
kuona kuna umuhimu wa kupata msaada wa madawati pamoja sare kwa wanafunzi wenye
mahitaji maalum.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Maendeleo, Ibrahimu
Mwangaraba amesema wanatambua umuhimu kama benki kuwa wanaowasaidia watakuwa
ni wateja wa benki yao,wengine ni viongozi mbalimbali ambao watasaidia maendeleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...