Mwanamitindo,Tausi Likokola akiwasili leo wa uwanja wa Ndege Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akitoke nchini Marekani kwa ziara ya siku 10 kushoto ni mama mdogo,Beatrice Likokola
 Mwanamitindo,Tausi Likokola akizungumza na waandishi habari (hawapo pichani) mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo Jijini Dar es Salaam.
Mwanamitindo Tausi Likokola akishiriki kucheza ngoma ya asili ya kundi la wanne Star mara baada ya kuwasili wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo Jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka)
               
 Na Chalila Kibuda
Mwanamitindo wa Kimataifa (Mtanzania) aishiye Ughaibuni, Tausi Likokola amesema Watanzania wanajitahidi mno katika tasnia ya mitindo, hivyo wanatakiwa  kuwa na ubunifu wa  kipekee kutokana kuwepo kwa ushindani katika tasnia hiyo.
Tausi ameyasema hayo mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam,amesma kwa miaka aliyoishi katika nchi za Ujerumani na Marekani, kwa sasa ndio ameona watanzania wakionesha ubunifu wao  ni mwanzo mzuri na wanaweza kufika mbali.
Tausi amesema anatarajia kufanya ushiriki wa shughuli za kijamii, kwani ndio wajibu wake kama mwanamitindo kutokana na kuwa mchango wake unahitajika katika jamii zenye mahitaji maalum.
Katika ujio wa Mwanamitindo huyo,Tausi anatarajia kutembelea  shirika lisilo la Kiserikali linaloshughulikia  watu wanaoishi na virusi (WAMATA) kutokana na kuwasaidia kwa kila hatua pamoja na kuzuru visiwa vya Zanzibar.
‘’Nimekuja katika ziara yangu hii nitafanya masuala ya kijamii lakini na uzinduzi wa mafuta ya marashi hapa nchini na nimeona uzinduzi huu ni ufanyie nchini kwetu iwe ni fahari yangu’’amesema Tausi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...