Na Chalila Kibuda.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limezuia maandamano ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Wananchi (JUVICUF) na kusema watakaoandamana
kesho  nguvu ya dola itatumika

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP),Suleiman Kova amesema wamewashauri vijana hao na kusema wataandamana hivyo ni lazima nguvu itumike kuzima maandamano hayo kutokana na kuzuia kufanyika kwa shughuli zingine.

Kova amesema kusudi la maandamano hayo ni ukiukaji wa haki za binadamu kwa jeshi la polisi pamoja na Tume ya Uchaguzi kuongeza siku za kuandikisha kutoka siku  saba hadi 14, ambapo waliwashauri kwenda huko kwa viongozi lakini wameshindwa kufanya hivyo na kuwataka wakate rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ili wafanye maandamano, nalo wamekataa.

“Mambo haya yote yakutaka kufanya maandamano yanazungumzika lakini wanataka kufanya hivyo ni lazima nguvu itumike kuzima kuacha kila mtu anafanya kitu anachotaka ni kufanya nchi isitawalike na sisi tunafanya nchi itawalike kwa watu kufuata taratibu”amesema Kamishina Kova.

Amesema kuwa Jeshi la  Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kesho wamejipanga katika kuhakikisha maandamano ya vijana hao hayafanyiki na watakaothubutu nguvu ya polisi itakuwa juu yao.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...