Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini 

Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini yalifanya mazungumzo  na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mjini Dar es Salaam jana.
Mazungumzo haya yalilenga kuandaa utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa mjini Arusha  mwezi wa januari tarehe 21 ambayo yanalenga kuyaunganisha makundi matatu katika chama cha SPLM kurudisha Amani na kuunda Serikali itakayowajumuisha viongozi kutoka makundi yote.
Katika mazungumzo ya jana makundi haya yamekubaliana kuendelea na mkakati  wa utekelezaji wa makubaliano ya Arusha kwa lengo la kuandaa utaratibu wa viongozi  wa makundi yote kurudi Sudan ya Kusini mapema iwezekanavyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...