IMG-20150203-WA0039
Waziri wa maji profesa jumanne maghembe akielezea utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa BRN chini.
....................................................

Waziri wa maji kupitia mpango wa BRN,kuanzia mwaka 2013 hadi sasa,imefanikiwa kuwafikishia maji wananchi milioni 4.3 wanaoishi maeneo ya mijini Aidha zaidi ya watu milioni 2 wanaoishi maeneo ya vijijini wamepatiwa huduma ya maji kupitia BRN.

Waziri wa maji profesa jumanne maghembe ameyasema hayo Februari 3, 2015 mjini Dodoma alipokuwa akizungumzia utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa BRN chini ya wizara ya maji katika ukumbi wa Fr.Vicent uliyopo ndani ya hotel ya St.Gasper

Profesa Maghembe amesema kuwa,mpango huo wa BRN umeonyesha kwa muda mfupi tofauti na ule mpango wa Taifa wa maji uliyonza mwaka 2017 hadi mwaka 2014,Amesema serikali kupitia mpango wa BRN itahakikisha inawafikishia wananchi maji katika maeneo mbali mbali ili kuwapunguzia kero ya maji.

Kadhalika Maghembe amewataka wafanyakazi wa mamlaka za maji hapa nchini kufanya kazi kwa kasi kubwa na sio mazowea,Katika mkutano huo viongozi wa mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira za miji mikuu ya mikoa zimetia saini makubaliano ya miradi ya maji na mazingira kwa kutumia utaratibu wa BRN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wananchi wamepata maji au mabomba ya maji?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...