Kampuni
ya ACACIA kupitia mgodi wake wa Buzwagi uliopo kwenye halmashauri ya
mji wa Kahama,imeipatia ushuru wa asilimia 0.3 (0.3%) ya mapato ghafi
halmashauri hiyo,ikiwa ni ushuru kwa kipindi cha miezi sita (Julai -
Disemba,2014) ambayo ni zaidi ya shilingi za kitanzania millioni
800,uliokabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama.
Kaimu
Meneja Mkuu wa mgodi wa Buzwagi ulio chini ya Kampuni ya ACACIA,Ing.
Mutereko Muganda (wa pili kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye
thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania millioni 800 kwa Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Bw. Felix Kimaryo (kulia) nje ya ofisi
ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Mh. Benson Mpesya (wenye tai).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...