Warsha ya wataalam wa misitu imeazimia kuwa kitajengwa Kituo cha Kuendeleza Misitu katika Nyanda za Juu Kusini ili kutoa mafunzo ya ngazi ya VETA kuhusu uendelezaji wa mashamba na viwanda vya misitu. Kituo hicho kitatoa mafunzo ya darasani pamoja na nje ya darasa kwenye misitu na viwanda.
Azimio hilo linasisitiza zaidi kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii, kupitia Programu ya Panda Miti Kibiashara, itahakikisha kuuundwa kwa Ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) kwa manufaa ya kituo hicho, na kuwa Umoja huo utamwajiri Mratibu ambaye ataongoza kituo hicho.
Sehemu ya Washiriki wa Warsha ya mambo ya Misitu wakiwa kwenye picha ya pamoja. |
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki, Bi Gladness Mkamba, mwishoni mwa Warsha ambayo ilifanyika Iringa katika kituo cha VETA tarehe 10 Machi 2015.
Warsha hiyo ambayo iliandaliwa na Programu ya Panda Miti Kibiashara ili kupokea na kuidhinisha taarifa ya mtaalam mwelekezi Bw Peter Shepherd kutoka Australia, kuhusu kukifufufa upya kituo cha Wafanyakazi wa Misitu kilichoko Sao Hill mkoani Iringa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...