Na Bashir Yakub.
Kumekuwa na shida sana hasa kwa upande wa wanaume kuwatelekeza watoto. Mara nyingi wanaume ndio hutelekeza watoto kuliko wanawake. Zipo baadhi ya kesi zimeripotiwa zikihusisha wanawake kuwatelekeza watoto lakini hizi si nyingi kama ilivyo kwa wanaume. Hii ni kwasababu uwezekano wa mwanaume kumkimbia mtoto ni mwepesi kuliko mwanamke kumkimbia mtoto/watoto. Jambo hili ni baya na limeshakemewa na sheria mbalimbali. Nataka niwaeleza kuwa kumtelekeza mtoto ni kosa la jinai.
Nikisema ni kosa la jinai maana yake ni kuwa kulifanya kwake kunahitaji adhabu ya kifungo jela au adhabu nyinginezo. Wapo watu hasa wanawake ambao wamekuwa wakitupiwa watoto na wanaume kwa makusudi. Ni ushauri wangu kwamba muda ni huu sasa kama ulikuwa hujui kuanzia leo ujue na uchukue hatua.
1.NINI MAANA YA KUTELEKEZA WATOTO/MTOTO KISHERIA.
Kutelekeza mtoto/watoto ni pamoja na kutotoa matumizi kama chakula, mavazi , matibabu, makazi, na mahitaji ya msingi( necessity) kama ada za shule, vifaa vya shule na kila kitu ambacho ni mahitaji ya msingi kwa makuzi na ustawi wa mtoto. Kwa hiyo mzazi asiyejihusisha kwa namna yoyote na huduma hizi nilizotaja kwa mujibu wa sheria huyu ndiye aliyetelekeza mtoto/watoto.
2.KUTELEKEZA WATOTO/MTOTO NI KOSA LA JINAI.
Sura ya 16 Sheria ya Kanuni ya Adhabu kifungu cha 166 kinasema kuwa Mtu yeyote ambaye, ni mzazi au mlezi au mtu mwingine mwenye uangalizi halali wa mtoto yeyote mwenye umri usiozidi miaka kumi na nne, hali ana uwezo, wakumuhudumia mtoto, kwa kuamua au kinyume cha sheria, au bila ya sababu za msingi akakataa kumhudumia, na akamtelekeza mtoto bila msaada, atakuwa ametenda kosa. Kwahiyo kumbe kutokana na sheria hiyo kumtelekeza mtoto ni kosa la jinai kama zilivyo jinai nyingine kama kuiba, kuua , kubaka n.k.
Aidha ni muhimu walioarhirika na matendo ya kutupiwa watoto wachukue hatua za kufungua kesi za jinai ili wahusika wawajibishwe.
Thubutu, sio wanaume wa Kitanzania hawatoi matunzo wala huwezi kuwapeleka mahakamani. Tuliona kesi ya IGP wa zamani aliyepelekwa mahakamani matokeo yake ilikuwaje?
ReplyDeleteSerekali ya siku hizi! Wanawake wengi maskini wamejichokea! Kila wanachojaribu wale wanaue wanaenda kuhonga na kuwatishia! nafikiri wengi wao wanasubiri tu Ukombozi wa Masia na sio serekali ya vyombo vyetu vya dola! Nothing called laws are enforced in Tanzania and if they are, is for the poor men who can not bribe and play the corruption crap!
ReplyDeleteMahousegirl walopewa mimba na kufukuzwa na watoto wao wako wapi? Walopewa mimba za bila mipango wako wapi???
nDUGU YAKUBU, HEBU TUPE UFAFANUZI KUHUSU KUMTUNZA MTOTO, NILIFIKIRI KUMTUNZA MTOTO NI JUHUDI ZINAZOUNGANISHWA NA PANDE MBILI YAANI MWANAUME NA MWANAMKE, LAKINI KATIKA MAKALA YAKO INAONEKANA KAMA MWANAMKE AHUSIKI KATIKA GHARAMA KAMA MALAZI, MAVAZI NA HATA CHAKULA, NAOMBA UFAFANUZI HAPO.
ReplyDeleteMBEGU
Hii sheria inafahamika kwa wale wachache wenye mwanga kidogo wa mambo ya sharia. Lakini wale ambao wako tayari kutoa ada ya tunzo ya motto kwa mwezi nikiasi gani? je inakidhi mahitaji ya mtoto kutokana na maisha ya sasa? Hili ni jambo la kuliangalia kwa undani. Nchi kama Botswana ukipitisha mwezi mmoja hujalipa wakiripoti utakwenda ndani,haijalishi cheo wala umaarufu wa mtu.
ReplyDeleteWewe bwana mbegu unataka ufafanuzi! Anasema wanaume wengi wamewateketeza watoto wao! Hawajui wanakula nini wanavaa nini wala wanasoma nini au wapi? SItaki kuleza zaidi lakni mimi ni mwanaume na nimeshudia marafiki zangu kiabo wao kueana mimba na binti sio ishu ila ishu ni binti akisema ana mimba atatukanwa, kupigwa na kudalilishwa kwa kila aina hapo anakata awasiliano kabisa! Sasa hao watoto mwenzetu aloacha huko barabarani nani anawalea! Mama zao kivipi? hajui wala haijulikani!?
ReplyDelete