Na Bashir Yakub.
Kumekuwepo na utata mkubwa kuhusu urithi wa mali za marehemu hasa inapotokea kuwa marehemu alikuwa na mke zaidi ya mmoja na hapohapo watoto wanaotokana na mama tofauti.
Tumeshashuhudia magomvi makubwa misibani lakini pia tumeshuhudia na tunaendelea kushuhudia utitiri wa mashauri kuhusu mkanganyiko wa mali za marehemu ambaye familia yake ni ya watoto wanatokana na mama tofauti.
Kutokana na hayo kuna umuhimu mkubwa wa kueleza sheria inasemaje kuhusu mazingira ya namna hiyo ili anayemua kuchukua hatua au kulalamika alalamikie kitu ambacho ni haki yake kweli na anayeamua kuacha aache akiwa ameridhika kuwa hajaonewa isipokuwa hicho alichopata ndiyo haki yake kisheria.
1.NINI MAANA YA MKE WA NJE YA NDOA.
Mke wa nje ya ndoa ni mke ambaye ameishi na mume kama mke na mume lakini akiwa hajafunga ndoa yoyote ya kiislamu, ya kanisani, ya serikali au ya kimila. Ndoa ya kiislamu hufungwa kwa taratibu za kiislamu ambazo huhusisha masheikh, makadhi n.k. Ndoa ya kikiristo hufungiwa kanisani na yaweza kufungishwa na mchungaji, askofu, padre n.k. Ndoa ya serikali hufungwa katika mamlaka za serikali kama kwa mkuu wa wilaya ubalozini n.k. Na ndoa za kimila ni ndoa ambazo hufungwa kutokana na mila na desturi za jamii fulani kwa mfano ndoa za kihaya, ndoa za kichaga n.k. Kwa hiyo kama mwanamke hana ndoa yoyote katika hizi basi yeye ni mke wa nje ya ndoa.
2. NINI MAANA YA MTOTO WA NJE YA NDOA.
Mtoto wa nje ya ndoa ni mtoto aliyetokana na ndoa isiyohalali au mahusiano yasiyo halali. Hapo juu nimetaja aina za ndoa halali. Hii ina maana kuwa iwapo mtoto amepatikana nje ya ndoa hizo basi huyo ndiye anayeitwa mtoto wa nje ya ndoa.
3. MKE ASIYE NA NDOA HARITHI.
Kwa mujibu wa sheria zetu hapa Tanzania zikiwemo tafsiri mbalimbali za sheria hizo ambazo hutolewa na mahakama kuu pamoja na mahakama ya rufaa mke wa wa nje ya ndoa hutambulika kama kimada. Neno kimada sio tusi isipokuwa ni neno la kitaalam linalomwakilisha mwanamke anayeishi na mwanaume bila ndoa na ndio maana neno hilihili limetumiwa na mahakama katika hukumu zake mbalimbali.
BOFYA HAPA Kusoma zaidi...
Sasa ndugu Bashir mbona unanichanganya, juzijuzi uliandika kwamba watu walili wakikaa pamoja kama mume na mke kwa miaka miwili basi hii ni ndoda halali hata kama hawajafunga ndoa kanisani, msikitini, serikalini au kijadi (cap 160). Sasa tuamini ipi?
ReplyDelete