WAANDAAJI wa Tamasha la Pasaka wamemualika Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi kushuhudia tamasha la mwaka huu.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari jana kuwa wamemualika Mzee Mwinyi kwa sababu ana historia kubwa na tamasha hilo.“Mzee mwinyi alikuwa mgeni rasmi kwenye tamasha letu la kwanza, hivyo tumemualika aje aone vijana wake tunavyoendelea baada ya kutupa baraka wakati huo.
 
“Bado hatujapata majibu, lakini naamini yatakuwa mazuri na atakuja kama mgeni wetu, maana tumealika wageni wengi sana wakiwemo viongozi wastaafu, viongozi wa sasa na makundi mbalimbali ya kijamii,” alisema Msama katika taarifa hiyo.
 
Mwaka huu Tamasha la Pasaka linatimiza miaka 15 tangu kuasisiwa kwake na Kampuni ya Msama Promotions ya Dar es Salaam na limekuwa likijiongezea umaarufu na kukubalika zaidi kutokana na ubunifu wake wa kufanya maadhimisho ya Sikukuu za Pasaka na Krismasi kwa umahiri na mguso wa kiroho kupitia matamasha hayo.
 
Umaarufu wa matamasha hayo pamoja na mambo mengine, unatokana na ukweli kuwa yamekuwa yakifanyika kwa ubunifu na umakini mkubwa huku kila mwaka yakiongezeka na kubadili waimbaji mbalimbali wa nyimbo za Injili wa ndani na nje ya nchi.
 
Baadhi ya nyota waliowahi kutumbuiza katika matamasha hayo ni marehemu Angela Chibalonza kutoka Kenya, nguli wa kutoka Afrika Kusini, Solly Mahlangu ‘Obrigado’, Sipho Makhabane na Rebeka Malope.
 

Wengine ni Ephraim Sekeleti kutoka Zambia, Ambassadors of Christ (Rwanda), Faraja Ntaboba na Solomoni Mukubwa (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo), 24 Elders  (Uganda) na Anastazia Mukabwa (Kenya).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...