MUIMBAJI nguli wa Kimataifa wa nyimbo za Injili, Rebecca Malope anatarajia kuwasili Jumaosi ya Aprili 4 akitokea Afrika Kusini kwa lengo la kupanda jukwaa la maadhimisho ya miaka 15 ya Tamasha la Pasaka.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo imekamilika kwa kiasi kikubwa hivyo mashabiki wa muziki wa injili hapa nchini kujitokeza kwa wingi kufanikisha tamasha hilo ambalo litakuwa ni la aina yake.

“Tamasha la mwaka huu lina mambo mengi ambayo yataendana na miaka 15 ya tamasha hilo kubwa hapa Tanzania kwa sababu linashirikisha waimbaji wa Kimataifa na viongozi wakubwa serikalini ambao hufikisha ujumbe wa serikali na neno la Mungu pia,”alisema Msama.
Msama alisema muimbaji Mtanzania anyeishi Kenya Faustine Munishi anatarajia kuwasili Aprili 3 kwa lengo la kufikisha ujumbe wa Neno la Mungu kupitia waimbaji na viongozi wa dini watakaojitokeza uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Hawa wanamuimbia Mungu hawaji kutoa Burudani!!!!???? Kulikoni? Hebu tuheshimu kazi ya Mungu jamani!
ReplyDelete