Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akisikiliza risala ya umoja wa wafanyabiashara wa Manispaa ya Sumbawanga iliyokuwa ikisomwa kwake na Mwenyekiti wa umoja huo Ndugu Willington Kiziba Ndyetabura (Kulia). Katika risala hiyo yalikuwepo malalamiko mbalimbali ikiwemo ya matumizi ya mashine za EFD ambapo ni pamoja na gharama kubwa za mataengenezo, Ada ya ukaguzi wa majanga ya moto(Fire), Kupanda mara mbili kwa kodi ya mapato kwa wafanyabiashara wadogo na Ulinzi na Usalama kwa wafanyabiashara. Wafanyabiashara hao walihoji n ivigezo gani vilivyotumika kupandishwa kwa kodi hiyo. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akizungumza na umoja wa wafanyabiashara wa Manispaa ya Sumbawanga tarehe 19/03/2015 katika mkutano wa pamoja wa kusikiliza kero zao mbalimbali uliofanyika katika ukumbi wa Upendo View katikati ya Mji wa Sumbawanga. Wafanyabiashara hao waliomba kuonana na Mkuu huyo wa Mkoa ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka wafanyabiashara hao kuwa wazalendo kwa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangia maendeleo ya Mkoa na taifa kwa ujumla.

 Katika kujibu kero zao mbalimbali alisema kuwa, zile kero ambazo haziwezi kutatuliwa mpaka yafanyike mabadiliko ya sheria atayachukua na kuyafikisha sehemu husika na pindi marekebisho yatakapohitajika yatafanyiwa kazi, aliwataka pia wafanyabishara hao watii sheria mbalimbali za kodi ikiwemo kuchangia ada ya ukaguzi wa majanga ya moto ili kuimarisha jeshi la zimamoto ambalo linahitaji maboresho makubwa kwa usalama wa wananchi na malizao.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...