Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Stephen Masatu Wasira amefanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe Mark Childress ofisini kwake.

Mhe Wasira katika mazungumzo yake na Balozi Childdress alibainisha changamoto zinazokabili kilimo nchini kuwa ni pamoja na zana duni zinazotumiwa na wakulima wadogo katika kilimo kuwa ni jembe la mkono. Alisema kwa kutumia jembe la mkono itakuwa ni ngumu kuondoa umaskini kwa wakulima wadogo katika maeneo ya vijijini.

Aliongeza kuwa jembe la mkono hutumiwa wakulima wengi wa vijijini katika uzalishaji wa mazao katika Taifa letu. ’’ Wakulima wadogo ndio tegemeo kubwa katika kuzalisha kilimo hapa nchini karibu asilimia 90 ya chakula hapa nchini inazalishwa na wakulima wadogo” alifahamisha Mhe Wasira katika mazungumzo yake.

Soko nalo ni tatizo lingine linalokabili mazao ya wakulima wetu wadogo waishio vijijini, alitoa mfano wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini katika mikoa ya Mbeya na Iringa ambako kuna mazao mengi na hasa mahindi ambayo yamekosa soko.

Pia ameiomba serikali ya Marekani kusaidia kuwekeza zaidi katika viwanda vya kilimo ili kuongeza thamani ya mazao ya wakulima wetu ili waweze kufaidika na juhudi zao na mwishowe waondokane na umasikini Uwekezaji katika viwanda vya kilimo utasaidia kuepukana na tabia ya kusafirisha malighafi na hivyo kutaongeza thamani ya mazao ya wakulima wetu, aliongeza Mhe Wasira.

Aidha, kitu kingine kilichosisitizwa na Mhe Wasira ni mkakati wa serikali kuwashirikisha vijana katika kilimo ili kuondokana na tabia ya sasa kwa vijana kukimbilia mjini na hasa Jijini Dar es Salaam kutafuta kile wanachokiita na kuamini kuwa maisha bora hupatikana mjini.

“ Kilimo cha Bustani ni muhimu kwani kinaweza kuwasaidia vijana kupata kipato cha haraka kwa kuwa mazao ya aina ya bustani huchukua muda mfupi kupata mafao yake, “ aliongeza Mhe Wasira.

Mhe. Wasira pia alisema serikali imejipanga kuhakikisha kuwa inaboresha kilimo cha umwagiliaji na akaiomba serikali ya Marekani kusaidia katika hili kwani itaongeza uzalishaji kwa wakulima wadogo kwa kuwa watazalisha mara mbili kwa msimu mmoja wa kilimo.

Wakulima wanasafirisha mazao ghafi nje ya nchi kama korosho bila kuongezwa thamani yake na hivi kuwakosesha kupata faida kubwa katika mazao yao. Naye Mhe Childress aliahidi kuwa serikali ya Marekani itafanyakazi na serikali ya Tanzania kuhakikisha kuwa inasaidia kilimo hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. The mdudu, sasa kama mnalijua hilo la kutokua na zana za kisasa kwenye kilimo kwanini mrikuja na kilimo kwanza? ...ok sawa mm yangu macho the mdudu huyo anaelekea morogoro kugombea ubunge kama mgombea huru nisie na chama.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...