Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja na Shughuli za Kanda wa Bohari ya Dawa (MSD),  Edward Terry (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ukumbi wa Idara Habari Maelezo jijini Dar es Salaam mipango ya MSD na mambo mengine. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa MSD, Etty Kusiluka.
 Etty Kusiluka akitoa ufafanuzi wa masuala kadhaa.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Dotto Mwaibale
WASIMAMIZI  wa vituo vya afya, zahanati, hospitali za wilaya, mkoa na hospitali za rufaaa wametakiwa kuwa makini katika kusimamia utoaji wa dawa na vifaa tiba ili kutoa matumizi ya dawa na vifaa tiba ili kuhakikisha vinatosheleza idadi ya watu katika eneo husika.

Wito huo ulitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa huduma kwa wateja na shughuli za kanda wa Bohari ya Dawa (MSD),  Edward Terry wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam katika ukumbi wa wa idara habari maelezo.

"Wasimamizi wa vituo vya afya na hospitali huleta maoteo ya dawa na vifaa tiba kulingana na idadi ya watu walionao kwenye maeneo yao na mara nyingi uangalia magonjwa yanayoshambulia zaidi maeneo hayo hivyo hakutakiwi kuwa na uhaba wa dawa endapo usimamizi mzuri utazingatiwa, alisema Terry.

Akitolea mfano wilaya ya Iramba, Igunga, Bariadi, babati , Arumeru na Sumbawanga kutokuwa na tatizo la dawa ambapo hufuata kanuni na sheria za uagizaji wa dawa kutoka bohari ya dawa pamoja na kutumia vyanzo vingine vya mapato kuongezea bajeti inayotolewa na serikali.

Pamoja na hilo  Teryy aliongeza kuwa usimamizi makini wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ndiyo utakaofanya changamoto ya ukosefu wa dawa kwenye hospitali na vituo kukoma.

"MSD imeboresha huduma na kumpatia mteja taarifa muhuimu zinazomhusu kwa kuziweka wazi taarifa hizo kwenye mtandao ambapo atapata fursa ya kupata taarifa hizo muda wowote.


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...