Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
IFIKAPO machi mwakani tatizo la umeme
jijini Dar es Salaam itakuwa historia kutokana na kukamilika kwa miundombinu ya mitambo ya umeme ifikapo machi mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini,George
Simbachawene katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya umeme ya Kurasini, Mbagala pamoja na Kinyerezi jijini Dar es Salaam leo.
Ziara hiyo iliyoanzia katika mitambo ya Umeme Wizarani
hapo na kuelekea,Kurasini na Mbagala ikiwa na lengo la kusogeza miundombinu ya umeme karibu na
watumiaji wa umeme.
Simbachawene amesema kuwa kuna miradi minne ambayo mpaka sasa
inafanyiwa kazi kwa uhakika
inayotegemewa kusambaza Umeme kwa watumiaji bila kuwa n amatatizo ya umeme.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO
Felshesm Mramba amesema kuwa matatizo
mbalimbali ya ununuzi wa Luku za umeme
nayo yanafanyiwa kazi kwa kuyahimiza
makampuni nayoshirikiana na TANESCO katika
uuzaji wa umeme ili waweze kuimarisha huduma hizo.
Waziri wa Nishati na Madini,George
Simbachawene akipewa maelekezo leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji
wa TANESCO Felshesm Mramba kuhusiana na uboreshaji
wa Mtambo wa umeme uliopo katika wizara
ya Nishati na Madini.
Waziri wa Nishati na Madini,George
Simbachawene akikagua Mtambo wa umeme uliopo nyuma ya jengo la Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
Mitammbo ya umeme iliyopo nyuma ya jengo la Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Liwe historia na maafisa usiku wapange na kuwekeza tukijua kuwa baada ya muda idadi ya watu inaongezeka na wanahitaji huduma, bila kuwekeza tukitarajia maendeleo na ongezeko la watu tatizo litajirudia miaka ijayo.
ReplyDelete