Na  Bashir   Yakub.

Ukisoma  kichwa  cha  habari  utaona  nimeongelea  nyumba  lakini    kimsingi   mchakato  huu  unahusisha  mali  zote  za  wanandoa  vikiwemo  viwanja,  magari,  na  kila  kitu  ambacho  ni  mali ya  wanandoa. Kichwa  kinajieleza  kuwa   ni  makosa  benki  au taasisi  yoyote  ya  fedha  kuuza   nyumba  au  mali  yoyote  ya  wanandoa  ikiwa  wakati  wa  kuchukua  mkopo  mwanandoa  mmojawapo  hakushirikishwa  katika    mchakato  wa  mkopo  huo. 

1.  MAANA   YA   MALI   YA  WANANDOA.

Mali  ya  wanandoa  ni  mali  yoyote  ambayo  imepatikana  kwa  nguvu   au  juhudi  za  pamoja  kati  ya  mme  na  mke  walio  kwenye  ndoa  ya  kikristo, kiislam,  ya  serikali  au  ndoa  nyingine  yoyote  halali  ikiwemo  ile  ya    kuishi  wote  kwa  muda  wa  miaka  miwili ( presumed  marriage ).  Hizi  zote  ni  ndoa   ambazo  mali  ikipatikana  ndani  yake  huwa  ya  wanandoa.  Pia  ile  mali   ambayo   mmoja  wa  wanandoa  amekuwa  nayo  kabla  ya  ndoa    lakini  baada  ya  ndoa  ikaendelezwa  na  wanandoa   kwa  kiasi  kidogo  au  kikubwa   nayo  hubadilika  kuwa  ya  wanandoa  wote. 

 Hii  inajumuisha  mali   zilizopatikana  kabla  ya  ndoa  lakini  wanandoa  wenyewe  wakaamua  kwa  hiari  yao  kuzifanya  kuwa  zao wote   kwa  pamoja  kama  familia kwa  makubaliano  maalum.  Nalazimika  kutoa  ufafanuzi  huu  ili ninaposema     mali  ya  wanandoa hairuhusiwi  kuuzwa  ieleweka  hata  kwa  kiwango  kidogo  mali  zipi  ni  za  wanandoa  na  hivyo  kuhitaji  ridhaa  ya wote  katika  kuwekwa  dhamana.

2.  MIVUTANO  KATI  YA  TAASISI  ZA  MIKOPO  NA   WANANCHI.

Kipindi  cha  hivi  karibuni  hasa  baada  ya  kuongezeka   wito  wa  ujasiriamali mali   na   wingi  wa  taasisi  za fedha   kumekuwepo na  kesi  nyingi  sana  kati  ya  raia  na  taasisi  hizi  za  fedha.  Unapoangalia  kesi  hizi   kwa  haraka  unaweza  kugundua  mambo   mawili,   kwanza    umakini  mdogo  wa  taasisi   za  fedha  hasa  katika   ufuatialiaji  wa  uhalali  wa  dhamana    na  pili  uelewa  mdogo  wa  raia  kuhusu taratibu   na  haki  walizonazo  katika  mikopo.  Raia  wanazilalamikia  taasisi  za  mikopo  kwa  kuwa  wababe , wasio  na  subira  na  wakiuka  taratibu  na  huku  taasisi  za  fedha  nazo  zinawalaumu  raia  kwa  kuwa  wakaidi ,wakorofi  na  wasiopenda  kurejesha  amana  wanazopewa.  Ni  msuguano mtupu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...