Na  Bashir  Yakub.

Sheria  ya  ardhi  ni pana   na  ina mambo    mengi.  Kila  nikipata  nafasi  huwa  najitahidi  kueleza  japo machache  ili   watu waweze  kuelewa  masuala  mbalimbali   kuhusu  ardhi.  Ardhi  ni  rasimali  nyeti  mno  na hivyo  ni  tatizo  kubwa   kuishi  bila  kujua mambo  ya msingi  na ya kisheria  kuhusu  ardhi. Kutokujua  ni  moja  ya  sababu inayopelekea  umaskini  wakati  utajiri  upo  mikononi  mwako na  upande  mwingine husababisha migogoro  ya ardhi  inayoongezeka  kila  kukicha  huku   watu  wakizidi  kupata  hasara. 

 Nimewahi kuandika  kuhusu  namna  ya  kisheria ya   kujua  iwapo  ardhi unayonunua  ina  mgogoro  au    hapana,  nikaandika  kuhusu  vitu  gani  viwe  ndani  ya  mkataba  wako  wa  manunuzi  ya  ardhi  ili  usitapeliwe na  mikataba  ya  ardhi  kwa  ujumla,   nikaandika  kuhusu  namna  nyepesi  ya  kubadili/kupata   hati/leseni  ya  makazi  unaponunua  ardhi   na  mengine  mengi  kuhusu  ardhi. Leo  naeleza  kitu  kingine  muhimu  katika  sheria ya  ardhi  ambacho  ni  dhamana(mortgages)    ambazo   unaweza  kutumia   kupatia  mkopo  iwapo  unahitaji  mkopo.   

1.NINI  MAANA  YA  DHAMANA.

Kifungu  cha  pili  cha  Sheria Ya  Ardhi   kinasema  kuwa  dhamana ni   hali  ya  mtu, taasisi  au  chombo  chochote  kuwa  na  maslahi  katika  ardhi  inayomilikiwa  na  mtu  mwingine  au  chombo  kingine, maslahi  ambayo   yanatokana  na  deni  au  mkopo.  Maana yake   ni  kuwa  ardhi  ni  yako  lakini  kitendo  cha mtu  mwingine  au taasisi  nyingine  kuwa na  maslahi   ndani  yake  na  maslahi ambayo  yanatokana  na kuwapo  kwa  deni  au  mkopo    basi hiyo  ndiyo  dhamana.  
Ieleweke  wazi  kuwa  dhamana  haihusishi umiliki  na  wala  haina  uhusiano na  umiliki. Dhamana  ni dhamana  na  mmiliki  anaendelea  kuwa  mmiliki.  Dhamana  haiondoi  haki  ya  umiliki( right  of occupancy).  

2.VITU  AMBAVYO   WAWEZA  KUWEKA   DHAMANA   NA  KUPATA  MKOPO.

Watu  wengi  wamekariri   kwa kujua   kuwa  dhamana  katika  masuala  ya  ardhi  ni  lazima  iwe  hati  ya  nyumba, barua  ya  toleo( offer)  au  leseni  ya  makazi.  Ni  kweli  vitu hivi  hutumika  kama  dhamana  lakini  si  hivi  tu  ambavyo  vyaweza  kutumika  kama dhamana.   Vipo  vitu  vingine ambavyo  vyaweza  kusimama  kama  dhamana    na  mtu  akapata  mkopo  kama ambavyo  tutaona  hapa.

(  A )  MKATABA   WA   PANGO.

Kisheria  mkataba  wa  pango  ni nyaraka  halali  ambayo  mtu  anaweza  kuitumia  kuombea  mkopo  katika  taasisi  ya  fedha.  Mkataba  wa  pango  ni  yale  makubaliano  ya  kawaida  kati  mwenye  nyumba  na  mpangaji. Mkataba  wa  pango  ni  nyaraka  muhimu  sana  japo  watu  wengi  huwa  hawaipi   uzito  zaidi  ya    kuamini  kuwa  inalinda uhusiano  kati  ya  mwenye  nyumba  na  mpangaji.  Ni  vyema  sasa  kujua kuwa  mkataba  wa  pango  hauishii  kulinda  mahusiano  ya   mwenye  nyumba  na   mpangaji tu  isipokuwa  ni  nyaraka ambayo   ikitumika  vyema  yaweza  kuwa    zana  ya  kukuza uchumi  wako.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...