Mkurugenzi
wa Tasisi ya Utafiti ya Ifakara,Salim Abdullah akisaini makubaliano ya
kuendeleza utafiti tasisi hiyo kulia ni Mkuu
wa Taasisi ya Kinga na wa China,Dk.Ning Xiao katika hafla iliypfanyika leo jijin Dar es
Salaam.(Picha Emmanuel Massaka).
WAZIRI
wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dk.Seif
Rashid akizungumza hafla ya makubaliano na Serikali ya watu wa China (
Kulia),Naibu Waziri na Kamisheni ya
Taifa ya Afya na Uzazi wa Mpango,na
Usimamizi wa Tiba Asili iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wadau mbalimbali wakishuhudia kutiliana saini kati ya Serikali na China katika suala zima la kuwekeza katika utafiti wa Tiba asili.
Na
Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
Serikali
imesema itaendeleza kufanya utafiti wa tiba asili ikiwa ni pamoja
na kuanzisha baraza la tiba asili ,kutokana na kuwepo kwa mafanikio ya
kutumia dawa hizo.
Hayo
aliyasema leo Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dk.Seif Rashid wakati akisaini makubaliano na Kamisheni ya Taifa ya Afya na Uzazi wa Mpango na Usimamizi wa Tiba Asili ya China,katika
kuendeleza Wizara ya Afya katika nyanja
ya utafiti,ujenzi wa kituo cha Moyo.
Amesema
makubaliano hayo yataongeza chachu kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, katika maeneo ambayo kwa
sasa Wizara imeongeza mkazo katika utafiti,hivyo kutokana na makubaliano yaliyofanyika kutaongeza kasi.
Dk.Seif
amesema kuwa madaktari kutoka nchini china wamekuwa wakija katika kutoa huduma
nchini hali ambayo inaonyesha ushirikiano katika sekta ya afya katika kuhudumia
wananchi.
Amesema
katika matumizi ya dawa za asili nchi ya China iko mbali ambapo wameweza kutoa
dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi.
Hata mnapowekeza huko msikubali wenye kutangaza matibabu mbadala kutangazao matangazo yanayosema dawa za hospitali ni sumu kwa sababu siyo kweli na hii inaweza kupotosha jamii.
ReplyDelete