Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum akisalimiana na mwakilishi kutoka UNICEF katika mkutano wa Lishe mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum akisikiliza kwa makini hoja iliyokuwa ikitolewa na mwakilishi kutoka CIFF katika mkutano wa Lishe mjini Washington DC.
Wajumbe kutoka nchi mbali mbali Duniani wakimsikiliza Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya ( hayupo kwenye picha) alipokuwa akiwasilisha mada na kuchangia hoja mbalimbali katika mkutano uliohusu Lishe bora kwa mtoto mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum akitoa mada na kuchangia hoja mbalimbali zinazohusu Tanzania katika mkutano wa Lishe mjini Washington DC.
Lishe bora ni msingi kwa ajili ya maendeleo
ya kiuchumi ya nchi.Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya
alipokuwa akiwasilisha mada katika mkutano ambao ulikuwa unazungumzia kuhusu
suala la Lishe (Nutrition).
"Ni muhimu
kuelewa madhara yatakayompata mtoto ikiwa mama hata mnyonyesha mtoto huyo ikiwa
ni pamoja na athari mbaya juu ya mwili na maendeleo ya mtoto kutoka mimba mpaka
kufikia umri wa miaka miwili kama mtoto
hatapat Madhara haya ni kubatilishwa.," Alisema Mkuya.
Mkuya aliongeza kuwa, “ Tanzania tunajitahidi
sana kupambana na janga hili kwani mama kushindwa kumnyonyesha mtoto kwa miezi
sita kunaweza kusababisha utapiamlo na kusababisha kuathiri mamilioni ya watu
katika Tanzania, hasa watoto, na hivyo kusababisha magonjwa kuenea na
kunyong’onyesha maendeleo ya kimwili na ki akili”.
“Kwa kuruhusu hali hiyo kunachangia kupunguza
uwezo katika kuboresha uwezo wakufikiri, kupunguza nguvu ya kujifunza na kuwa mbunifu, kuongezeka kwa
umaskini, na kasi ndogo katika kufikia maendeleo ya kijamii na
kiuchumi”.Aliongeza Mkuya.
Takwimu za mwisho za utafiti wa mambo ya afya
zina onyesha kuwa asilimia 59 ya watoto
wenye umri wa miezi 5-59 wana upungufu wa madini,asilimia 33 ya watoto chini ya
miaka sita wana upungufu wa vitamin A. Asilimia
11 ya wanawake wenye umri wa kuzaa yaani
miaka 15-49 wana uzito wa chini, asilimia 41 wana uzito wa chini na
upungufu wa madini, wakati asilimia 58 ya mama wajawazito wana upungufu wa
madini pia.
“Katika Tanzania mikoa ambayo inafanya vizuri
katika kupambana na utapiamlo ni mkoa wa Kilimanjaro, Mjini magharibi na Mkoa
wa Dar es salaam.” Alisema Mshauri Lishe wa Rais Jakaya Kikwete”.Dr. Wilbald
Lori.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo
zinakabiliwa na janga hili, hivyo katika mikutano hii mikakati mbalimbali inapangwa
ya jinsi ya kulimaliza kabisa tatizo hili.
Mikutano hii bado inaendelea na hali ya hewa
mjini hapa ni baridi kiasi.
Imetolewa na
Msemaji :Wizara
ya fedha
Ingiahedi
C.Mduma
Washington DC
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...