Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
 WANANCHI watatu kati ya kumi  wameshakumbana na  wizi ndani ya kipindi cha mwaka  jana,na asilimia 84 ya wananchi  wanaamini kuwa kuna uwezekano wa kuathiriwa na makundi ya vijana waharifu kama panya road.

 Hayo yameelezwa kwenye Utafiti umefanywa na Twaweza kwenye utafiti wenye jina la Je, tuko salama? maoni ya wananchi juu ya usalama na haki waliofanya mkutano katika ukumbi wa mikutano  wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam leo.
Mtafiti wa twaweza Elvis Mushi amesema kuwa licha ya kuongezeka kwa matukio ya vurugu za kisiasa pamoja,wizi na hofu juu ya makundi ya vijana ya wahalifu wananchi wengi  wamekuwa  hawana  usalama wao katika maisha wanayoishi.
 Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza  Aidani Eyakuze aliongezea kuwa  kwanza wananchi wengi wanahisi kuwa salama maeneo yao lakini bado wanakumbana na vitendo vya wizi, wanaogopa kuvamiwa na panya road na baadhi yao   kushuhudia ghasia na vurugu za kisiasa. 

Aidha watu wameshuhudia ongezeko la ukatili dhidi vya vituo vya polisi ndani ya miaka miwili iliyopata, jambo hili linapunguza imani yao na vyombo vya usalama.  
 Eyakuze aliongeza kuwa usalama una umhimu wa kipekee katika masuala ya kijamii na kiuchumi akiwa na akiwa na rai kwa serikali  kuyazungatia maoni haya ya wananchi katika utekelezaji wa jukumu lake la kuwahakikishia wananchi usalama wa hali na mali.
Ofisa masoko wa Twaweza Costantine  Magavilla akizungumza leo na wajumbe kutoka makampuni mbalimbali katika mkutano wa Twaweza uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Makumbusho ya Taifa  jijini Dar es salaam,(kulia) ni Mtafiti wa Twaweza Elvis Mushi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza Aidan Eyakuze akiuliza swali kwa wajumbe waliohudhuria katika mkutano wa Twaweza leo katika ukumbi wa mikutano wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es salaam  kushoto ni Mkurugezi wa Capacitate Consulting, Ngasuma Kanyeka.
 Baadhi ya wajumbe kutoka makampuni mbalimbali waliohudhuria mkutano wa Twaweza katika ukumbi wa mikutano wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Mstaafu) (CAG), Ludovick Uttoh akizungumza na baadhi ya wandishi wa habari katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam leo. (Picha zote na Avila Kakingo,Globu ya Jamii).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...