Mkurugenzi
Mtendaji wa Mfuko Sekta Binafsi Nchini (TPSF),Godfrey Simbeye akizungumza na
waandishi wa habari katika warsha iliyowakutanisha wafanyabiashara wa China na
Watanzania iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es
Salaam.
Mwenyekiti
wa Baraza la Biashara la China na Afrika
(CABC) Tawi la Tanzania,Xian Ding akizungumza na waandishi wa habari katika warsha iliyowakutanisha wafanyabiashara
wa China na Watanzania iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini
Dar es Salaam.
Sehemu
ya wadau katika katika warsha iliyowakutanisha wafanyabiashara wa China na Watanzania
iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam.
Na
Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Mfuko Sekta Binafsi Nchini (TPSF),Godfrey Simbeye amesema kukutana
na watu wa China ni fursa nzuri ya watanzania katika kushirikiana katika sekta ya
uwekezaji nchini.
Simbeye
amesema hayo katika warsha iliyowakutanisha wafanyabiashara wa China na
Watanzania iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es
Salaam.
Simbeye
amesema wachina hawaji Tanzania kutembea bali wanakuja kwa ajili ya kukuza
viwanda vyao vilivyopo nchini ,hivyo ni fursa kwa wawekezaji watanzania kuweza
kukutana na wachina hao ili kushirikiana nao.
Naye
Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la
China na Afrika (CABC) Tawi la Tanzania,Xian Ding amewataka wachina pamoja na
watanzania kuzidisha ushirikiano ili kupata maendeleo katika biashara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...