Pichani ni baadhi ya wakazi wa maeneo mbali mbali ya jiji la Dar, wakiwa kwenye foleni ya kununua umeme wa luku kwenye kituo cha Sayansi, Kijitonyama baada ya kupatwa na kwikwi kwa siku kadhaa zilizopita kwenye vituo vingine pamoja na kwenye mitandao ya simu.ila sasa Tanesco wametoa taarifa na kusema mambo yako mswano kwa sasa.

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO) 
 TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA LUKU KWA BAADHI YA MAWAKALA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatoa ufafanuzi juu ya tatizo lililojitokeza kwa baadhi ya mawakala wa LUKU kushindwa kutoa huduma ya kuuza umeme. Hali hiyo inatokana na Kampuni ya Selcom ambaye ni wakala wa kuuza na kuyaunganisha baadhi ya makampuni ya simu kwa Tanesco kusitishiwa huduma kutokana na kushindwa kutekeleza baadhi ya majukumu yake kimkataba.

Wakati suala hili likiendelea kushughulikiwa na mamlaka zinazohusika tunapenda kuwahakikishia wateja wetu kuwa, huduma zinaendelea kupatikana kupitia Kampuni ya MAXCOM katika Vituo mbalimbali, ATM za CRDB na NMB, NMB Mobile pamoja na ofisi zote za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) nchi nzima hadi siku ya Jumamosi na Jumapili na siku za Sikukukuu kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 03, 2015

    Litatoa ufafanuzi!! Yaani kwa sasa hawana maelezo yoyote? Mpaka wakakae na kupanga vipi wazuge? Tanesco hawana credibility yeyote ile. Uwongo ndio mbinu za maelezo yao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...