Katibu wa Bunge Dkt. Thomas kashililah akisisitiza jambo wakati alipokutana na ujumbe kutoka taasisi inayojishughulisha na masuala ya kibunge ya Parliamentarians for Global Action Ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo upo kwenye ziara yao ya kikazi kutembelea kila Bunge Duniani na kueleza malengo na mipango yao hususani kuangalia namna wanavyoweza kushirikiana na wabunge kutatua baadhi ya masuala yahusuyo haki za Binadamu. Kulia ni Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Ndg. John Joel, na kushoto ni Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Jossey Mwakasyuka na Msaidizi wa Katibu Ndg. Emmanuel Mpanda.
Katibu Mtendaji wa taasisi ya Parliamentarians for Global Action yenye makao makuu yake Mjini New York Marekani Dkt. David Donat Cattin akielezea baadhi ya shughuli za taasisi yake alipokutana na Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah (hayupo pichani) Ofisini kwake jana Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Kimataifa la Taasisi hiyo Duniani Mhe. Pindi Chana.
Katibu Mtendaji wa taasisi ya Parliamentarians for Global Action yenye makao makuu yake Mjini New York Marekani Dkt. David Donat Cattin akielezea baadhi ya shughuli za taasisi yake alipokutana na Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah (hayupo pichani) Ofisini kwake jana Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Kimataifa la Taasisi hiyo Duniani Mhe. Pindi Chana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2015

    Picha ya pili anayezungumza ni Mhe. Yussuf Abdallah Nassir, Mbonge wa Korogwe Mjini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...