Na Sultani Kipingo 

Mahakama nchi Spain imeamuru mgomo wa wachezaji nyota nchi hiyo uliopangwa kufanyika Jumamosi wakipinga sharia mpya ya haki za mapato kwenye TV, hivyo ndio kusema fainali timu ya Barcelona itaweka msumali wake wa mwisho wa La Liga dhidi ya Atletico Madrid siku ya Jumapili.

Mahakama hiyo ya National Court imesema katika uamuzi wake leo kwamba kuruhusu mgomo huo uendelee kutazuia kumalizika kwa michuano ya ubingwa ya nchi hiyo na pia kusababisha mvurugano mkubwa wa kiutawala. 

"Mgomo huo utavuruga mikataba ya kimataifa ya Spain na vilabu vyake, kadhalika na likizo za wachezaji”, Mahakama hiyo imeongezea. 

Muungano wa wachezaji nchini Spain (AFE) ulitangaza wiki iliyopita kwamba wachezaji watagoma kuanzia Jumamosi na uongozi wa La Liga uliweka pingamizi na kuuita mgomo huo kama kinyume cha sharia. 
Mgomo huo, unaoongozwa na nyota wakubwa kama Iker Casillas wa Real Madrid na Adres Iniesta wa Barcelona, una nia ya kushinikiza kwamba vilabu vidogo vipatiwe donge kubwa Zaidi kutoka mapato yanayotokana na haki za kuonesha michezo kwenye TV. 
Mahakama hiyo imesema uamuzi wa kuzuia mgomo huo ni hatua ya muda mfupi wakati ikiendelea kuipitia kesi hiyo, na hukumu itatolewa Juni mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...