Na  Bashir  Yakub.
Siku  zote  wananchi  wamekuwa    wakililalamikia jeshi  la polisi  kwa  namna  linavyoendesha  shughuli  zake hasa wakati  wa  ukamataji (arrest). Matumizi  ya  nguvu, ubabe    na  kutofuata  sheria    na  taratibu  maalum  limekuwa  ndio  tatizo  kubwa  kwa  wananchi  dhidi  ya  askari.  

Sio  siri  askari wamekuwa  wakitumia  nguvu  na  ubabe  mno  katika  kuwakamata raia.  Hata  pale pasipo  na  haja  yoyote  ya  kutumia  nguvu    bado  wao  wamekuwa  wakilazimisha  nguvu  nyingi  hali  ambayo  hupelekea   vurugu , kuumizana  na  hata  mauaji. Mara  nyingi  unapochunguza  matukio   mbalimbali  ya  vurugu ambayo  huwahusisha raia  na polisi  utagundua  kwa haraka kuwa  ubabe    wa askari  ndio  uliopelekea  vurugu.  Basi  leo  nitaeleza nini  ufanye  askari  anapokiuka  taratibu   hasa  wakati  wa  kukamata/kuweka  chini ya ulinzi.

1.NINI  MAANA  YA  KUKAMATA ( ARREST ).
Sura  ya  20  Sheria  ya  Mwenendo  wa  Makosa  ya  Jinai  kama  ilivyofanyiwa  marekebisho  2002  ndiyo  sheria  inayotoa  mwongozo   wa  namna  na  jinsi  ya  kumkamata  mtu.  Pamoja  na  hayo sheria  hii  haikueleza   moja  kwa  moja  nini  maana  ya  kukamata. Hata  hivyo  kutokana  na  miongozo mbalimbali  ya  kimahakama  ambayo  hutumika  kutafsiri  sheria  hii  tunaweza  kupata  tafsiri  ya  neno  kukamatwa  kwa  kusema  kuwa  ni  tendo  la  kumzuia  kwa  muda   raia  ambaye  inatuhumiwa  kwa  kosa  fulani,   ambalo  hufanywa  na  mamlaka  husika. 

Kwa tafsiri  hiyo  tendo la kuzuia  lazima  liwe    la  muda,  raia  anayekamatwa  lazima awe  ametuhumiwa, na pia  ukamataji  lazima  ufanywe  na  mamlaka.  Huo  ndio  utakuwa  ukamataji ( arrest).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...