Na Bashir
Yakub.
Malalamiko ya
raia dhidi ya
jeshi la polisi
hayataishi kama polisi
wenyewe hawatajirekebisha. Na
ieleweke kuwa si kweli
kwamba wanaolalamika ni wajinga
au hawana sababu za msingi.
Mara zote ukiangalia
malalamiko ya raia huwa
ni ya msingi na
mzizi wake ni mmoja
tu. Ni utamaduni
wa askari wetu kutopenda kutenda
hatua kwa hatua
kama sheria inavyoagiza. Sheria imetoa
maelezo mazuri tu ya
namna ya
kuyaendea mambo. Tatizo watekelezaji
ndio hakuna.
Sheria husema
kingine na watekelezaji
hufanya kingine. Namna hii
huwezi kuepuka chuki
na migongano kati
ya hawa watekelezaji
askari na raia. Na
migongano na kutokuelewana kunapokuwa
kukubwa na usalama
nao unayumba kwakuwa
ili askari afanye
kazi ya usalama
vizuri anategemea msaada
wa raia karibia
kwa asilimia zaidi
ya 80. '
Na
raia huyu hatatoa ushirikiano
wakati jana umempiga
bila sababu, umemtukana
na kumtolea maneno
ya kebehi. Makala iliyopita
nilizumgumzia namna sheria
inavyomruhusu raia kukataa
kukamatwa na polisi
iwapo polisi huyo
atakiuka taratibu katika
ukamataji. Leo nazungumzia
namna sheria inavyokataza kumchukua mtu
mwingine baada ya
kumkosa mtuhumiwa halisi
wa kosa. Tutaona
hili likoje.
1.ASKARI KUONDOKA
NA MTU MWINGINE
BAADA YA KUMKOSA
MTUHUMIWA HALISI.
Hii ni tabia
ambayo imezoeleka sana
na ipo kwa
muda mrefu. Yumkini kuzoeleka
kwake na kuwepo
kwake kwa muda mrefu hakuifanyi hata kwa sekunde
moja tabia hii kuwa halali
kisheria. Mara nyingi
wanaokutwa sana na tabia hii
ni watu wa vijijini hasa
wa hali ya chini. Lakini
hata mijini pia
ipo sana. Nazungumzia
tabia ya kuondoka
na mtu mwingine
baada ya kumkosa mtuhumiwa halisi.
Kwa mfano askari
wamekuja nyumbani kumtafuta
JOHN kwa kosa
analotuhumiwa nalo. Bahati
mbaya au nzuri
JOHN hayupo nyumbani.
Kutokana na hilo askari
wanaamua kuondoka na
mke wa JOHN
au mtoto wake
ili kumfanya JOHN
aweze kutokea. Hiki ndicho
ninachozungumzia. Na wanaokuwa wakichukuliwa
mara kwa mara ni
mke wa mtuhumiwa
, mtoto au ndugu. Lengo
eti ni kumfanya mtuhumiwa
halisi aweze kujisalimisha.
SOMA HAPA ZAIDI
SOMA HAPA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...