Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali wa
Dkt. Servacius Likwelile akiwa pamoja na Kamishina wa Fedha za Nje Bw.
Ngosha Magonya wakati mara tu baada ya kuwasili katika uwanja wa
ndege mjini Abidjan.
Akizungumza na vyombo vya habari mchana huu DKt.Likwelile ambaye ni
amemuwakilisha Waziri wa Fedha na katika Mkutano wa Benki ya Dunia
amesema kuwa,”Mkurungezi wa Kanda ametoa ripoti ya mwaka,
ameelezea ni namna gani ukanda huu wa Afrika ulivyokuwa ukifanya kazi
za maendeleo, ameelezea ripoti hiyo kuwa inagusa nchi zote sita za
Afrika. Nchi hizo ni pamoja na Rwanda, Tanzania,Uganda, Kenya,
Ethiophia na Visiwa vya Shelisheli, Aidha nchi hizo zimefanya kazi vizuri.
Alisisitiza Likwelile.
Likwelile amefanafua kuwa, “Mkurugenzi wa ukanda wanchi za Afrika
ameelezea jinsi uchumi unavyokua kwa kasi kubwa kwani umekua kwa
asilimia sita mpaka saba na ukuaji huu wa uchumi unawanufaisha watu
wote wa nchi hizo.
Ni Muhimu kuwekeza kwenye reli hii itawapunguzia wananchi usumbufu
wanaoupata kwenye masuala ya usafiri na usafirishaji wa mizigo.Aliongeza
Likwelile.
Pia Likwelile amezungumzia kuhusu kuendeleza kilimo hasa kilimo chenye
tija. alisema kuwa kilimo cha biashara humuongezea kipato mwananchi
wa chini na kumfanya kujikwamua kwenye hali ya kimasikini.
Aidha mwenyikiti amezungumzia suala nishati hasa nishati ya umeme ili
tuweze kuendelea ni muhimu kusimamia suala la umeme kwa kikanda. Hii
itapelekea nchi zote za Afrika kunufaika na masuala ya maendeleo
kiujumla kwa nchi hizo za kikanda.
“ Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa rais, Aidha ukanda wa nchi
za Afrika unapenda kumshukuru raisi aliyepita Dkt. Kaberuka kwa kazi
nzuri aliyoifanya kwani ameziacha nchi katika hali nzuri sana” Alisisitiza
Likwelile.
Mwisho Likwelile alifafanua kuwa, “Benki ya Maendeleo ya Afrika
imetambua umuhimu wa kazi na mchango mkubwa alioutoa Mhe. Jakaya
Mrisho Kikwete na ndio maana imemualika katika Mkutano huu wa mwaka
kutokana na kazi zuri aliyoifanya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...