Na Bakari Issa Majeshi
Mgomo wa Madereva uliodumu  kwa takriban siku moja na ushee, hatimaye umepata muafaka baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Paul Makonda (pichani) kufanikiwa kuusuluhisha kwa kusaini makubaliano na Uongozi wa Chama cha Madereva.
Makubaliano hayo yaliitaka Serikali kuboresha  Mikataba kwa Madereva, malipo kwa madereva hao, pamoja na tatizo la ukaguzi wa magari ili kuondoa usumbufu kwa madereva hao, na kuiomba Serikali kufanya ukaguzi huo kwa siku moja tu.
Akizungumza na Madereva hao, Mhe, Makonda amewataka Madereva hao kuachana na mgomo huo  na kuwaahidi Madereva hao kuyafanyika kazi madai yao katika muda ambao wamekubaliana usiozidi saa 4 asubuhi kesho.

Aidha, Mhe Makonda amesema katika madai hayo imeundwa Tume ambayo itashughulikia madai hayo pamoja na kuwahakikishia Madereva hao kuwepo na mwakilishi katika Tume hiyo iliyoundwa, ambayo itajadili masuala ya Mkataba, malipo, matibabu pamoja na suala la kusoma kwa Madereva hao.
Pia Makonda amelitaka Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni kuwaachia Madereva ambao tayari walikua wamekamatwa kutokana na kuonekana kufanya fujo katika mgomo huo katika Soko la Urafiki jijini Dar es Salaam. 
Kwa Upande wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Madereva, Bw. Rashidi Salehe amemuomba Mkuu wa Wilaya kutatua madai ya Madereva hao ili kuondoa mgomo ambao unakwamisha usafirishaji wa abiria.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZA HALI ILIVYOKUWA 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 05, 2015

    Duh!.hivi mkuu wa wilaya anayo mamlaka ya kuliambia jeshi la polisi kumwachia mtu aliyevunja sheria? Si Tz mnafata sheria na utawala bora?siamini khaa!!

    Sipati picha ikitokea hapa marekani sijui watu wagome/waandamane kutetea uhalifu halafu rais ..aje aseme waachiwe huru?kwa maneno???duh.!kweli bongo Tambararee!

    mdau
    Washington DC

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 05, 2015

    Afadhali suluhisho hili ni afueni kwa wasafiri.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 05, 2015

    Katika conflict mitigation hiyo ni possible. Wanaachiwa kumaliza tatizo. Ni common practice sehemu nyingi duniani

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 06, 2015

    Sielewi unaposema serikali iboreshe mikataba ya madereva, na malipo yao. Kwani mwajiri wao ni serikali?!

    ReplyDelete
  5. mweee! wadau munaochangia kwa kuongea na kiingereza na kuswahili munatuacha njia oanda khaaa! . Ongeeni lugha moja ilituwaelewe basi moja kwa moja sio munatuchanganyia lugha. asante. Mimi Andrew Chale Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...