Na  Bashir  Yakub.

Ni  jambo  la  kutia faraja  kuwa   vijana wengi  wamekuwa  wajasiriamali   na wanafanya  biashara  mbambali   katika    maeneo mbalimbali  ya  nchi. Wengine  biashara  ni  nzuri  na  wengine  wanalalamika  biashara  sio  nzuri. Kila  mtu  ana  muono wake   kuhusu  mwenendo  wa  biashara  zake. 

 Pamoja  na  hayo  ushahidi  wa  sayansi  ya  biashara  unathibitisha  kuwa  kwa  asilimia  zaidi  ya  70  suala  la biashara  kuwa  mbaya   au  nzuri  hutokana  na  mtu  mwenyewe alivyojipanga. Mbinu, umakini, mtaji, uendeshaji, mipango,  na  weledi.  Nilipoandika  kuhusu  njia au namna  ya kuunda  kampuni  nilieleza  kuwa  masuala  ya  uendeshaji  wa  kampuni   huwa  ni  masuala  ya  kisheria. Kila  kitu  katika  kampuni  ni sheria  kuanzia  usajili, uendeshaji    mpaka  kufa  kwa  kampuni .

 Ni  kwa  maana  hii  nasema  kuwa  mjasiriamali   anapopata ushauri   mzuri  wa  masuala  mbalimbali  ya  sheria  katika  uendeshaji  wa  kampuni  basi  yaweza kuwa  nafasi  ya  ustawi wa  kampuni.  Leo  nazungumzia kitu  kingine  cha  kisheria  katika  uendeshaji  kampuni kiitwacho  mikataba  kabla  ya  kampuni ( pre  incorporation contracts). Tutaona  hapa chini  maana  na  umuhimu  wa  kujua  kitu  hiki.

1.NINI  MAANA  YA  MIKATABA  KABLA  YA  KAMPUNI ( PRE  INCORPORATION  CONTRACTS ).

Mikataba  kabla  ya  kampuni   ni  kama  jina  lenyewe  linavyojieleza.  Hii  hujumuisha  biashara  alizokuwa  anafanya  mtu  kabla  ya  kuwa  na   kampuni lakini baadae  akawa  na  kampuni   na  akaendeleza  biashara  zilezile. Watu  wengi  ambao  tayari  wameanzisha  makampuni   hujikuta  walikuwa  na  biashara  zao   hata  kabla  ya  kuunda  makampuni hayo.  Pengine  kutokana  na  biashara  kupanuka  mtu  anaamua  kuunda  kampuni   ili  kuendeleza biashara  ileile.  Kwa ufupi  maana  ya  hili  ni   kuwa,  ni  ile   biashara   aliyokuwa  nayo  mtu    na  kuamua  kuiundia  kampuni . 

Mtego ( technique)   wa  kisheria  uliopo  hapa ni  kuwa  umekuwa  na  biashara  ambayo  haikuwa  kampuni ,  ina  maana  katika  biashara  hiyo  umefanya  mikataba  mbalimbali  kwa  mfano  umefanya  mkataba  wa  pango au   mkataba  wa  manunuzi ya  eneo  la  biashara, umekuwa  ukinunua  bidhaa  mbalimbali   kwa  kuandikishana  au  kupewa  risiti( risiti nayo ni  mkataba),mikopo  mbalimbali,  ulinunua mali  mbalimbali  kwa  ajili  ya biashara  zako  kwa  mfano  gari, pikipiki, baiskeli  au  maguta  kwa  ajili  ya  kubebea  mizigo n.k  Hii  yote  ni  mikataba  uliyoifanya  kabla  ya  kuunda kampuni  na  ndio  huitwa “pre incorporation  contract”.

 Swali  ni  je  utakapounda  kampuni  na  biashara  hiyo  yote  na  mali  zake kuziweka  chini  ya  kampuni , mikataba  hiyo  itakuwa  inaibana  kampuni  na  je kampuni  inawajibika  kwa  lolote  litakalotokana  na  mikataba  ambayo  imeingiwa  kabla  ya  kuundwa/kuzaliwa kwake ?. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...