MWAKILISHI viti maalumu wanawake CUF wilaya ya Chake Chake, Mhe. Salma Mohamed Ali (kulia) akimkabidhi dawa na vifaa tiba,   Daktari dhamana wa hospitali ya Chake Chake, Dk. Yussufu Hamad Idd vilivyotolewa na mwakilishi wa Jimbo la Chake chake, Mhe. Omar Ali Shehe, Mei 3 mwaka huu, kabla ya baadhi ya vifaa na dawa hizo kugunduilika kupitiwa na muda wake wa matumizi.
BAADHI ya dawa na vifaa tiba zilizotolewa hivi karibuni na Mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake, Mhe. Omar Ali Shehe ambazo tayari zimeshapitiwa na muda wake wa matumizi, ambapo uongozi wa hospitali ya Chake chake umezigundua wakati wakitaka kuzitumia.
MFAMASIA mkuu wa hospitali ya Chake Chake Pemba, Dk.  Kassim Zahir akionyesha vipamba vya kusafisa damu baada ya kung’olewa jino, ambavyo navyo ni miongoni mwa vifaa tiba vilivyogundulika kupitiwa na muda wake, ambavyo vilitolewa hivi karibuni na Mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake, Mhe. Omar Ali Shehe, pamoja na dawa nyengine.
DAKTARI dhamana wa hospital ya Chake Chake Pemba, Dk.  Yussuf Hamad Idd, akitoa maelezo jinsi watakavyomkabidhi dawa na vifaa tiba Mwakilishi wa Jimbo la Chake chake, Mhe. Omar Ali Shehe ambaye hivi karibuni alikabidhi dawa hizo ambazo zimegundulika kupitwa na muda wake wa matumizi.(Picha na Haji Nassor, Pemba).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...