Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band almaarufu kama FFU-Ughaibuni yenye maskani yeke nchini Ujerumani,siku ya jumamosi 30 Mei 2015 bendi hiyo italitingisha hekalu la Uebersee Museum mjini Bremen,kuanzia Saa moja Usiku hadi kumekucha. 

Onyesho hilo la usiku usiokwisha limeandaliwa na utawala wa hekalu hilo la makumbusho la Uebersee Museum,ambapo utawala huo umeiomba bendi ya Ngoma Africa band kwenda kutumbuiza,kwa kuwa bendi hiyo ilitumbuiza mwaka 2013 na  kuvunja rekodi ya kuwavuta washabiki wengi kuliko bendi yeyote katika historia ya matamasha yafanyikao katika hekalu hilo.
Ngoma Africa band inayoongozwa na kamanda  Ras Makunja ni bendi pekee ya kiafrika yenye mvuto mkubwa barani ulaya,na washabiki wake wameipachika majina mengi ya kiusanii kama vile FFU-Ughaibuni,Viumbe wa ajabu  ANUNNAKI Alien's (himaya ya mazimwi wa Anunnaki), pia maarufu kwa majina kama Mzimu wa Muziki,na "Watoto wa Mbwa" . 

Ngoma Africa band pia inatajiri wa wanamuziki wenye vipaji vya hali ya juu wakiwemo yule mpiga solo mahiri Afande  Chris Bakottesa aka Afande Chris-B, Sanjint major Jo jo Sousa, wanamuziki chipukizi wengi walizalishwa na bendi hiyo ambayo inawanamuziki kumi.

Ngoma Africa band ilianzishwa mwaka 1993 na kiongozi wa bendi hiyo ambaye pia ni mtunzi wa nyimbo nyingi za bendi hiyo Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja.
unaweza kuwasikiiza FFU


unaweza kujumuika nao pia at ngoma4u@gmail.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 26, 2015

    Jina la WATOTO WA MBWA walipewa na mgombea urais wa chama kimoja cha upinzani 2010 kwa kuwa walimbwakia kwa kupitia kituo kimoja cha redio,Mzee yule hakuwavumilia akamua kuwapa jina la WATOTO WA MBWA

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 26, 2015

    Si mchezo ffu wanatisha wanapotuachaga midomo wazi ni yale madongo katika nyimbo zao

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 26, 2015

    FFU -ughaibuni aka wazee wa gwaride jamaa awapendagi kulemba wao ni mbele kwa mbele tu

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 26, 2015

    Kikosi kazi chini ya kamanda mkuu aliyeipindia akili kazi yake

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...