Watangazaji wa Clouds FM kupitia kipindi cha Powerbreakfast Gerald Hando pamoja na Hudson Kamoga wa Clouds TV kupitia kipindi cha Clouds 360 wakifanya mahojiano na Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini na kwingineko Diamond Platnum akiwa na mchumba wake Zari the bosslady,kuhusiana na mambo mbalimbali yakiwemo ya maisha yao na pia kuhusu onesho lao la Zari White Party wanalotarajia kulifanya usiku wa leo pale Mliman City,Jijini Dar.
Onesho hilo ambalo lilizua gumzo kila kona ya jiji la Dar likijulikana kwa jina la The White Party leo ndio kilele chake,kiingilio chake ukikisikia lazima usisimke,Kiingilio cha Onesho hilo kimevunja rekodi,haijawahi kutokea,kwa maana ya kwamba kiingilio kimepangwa kwa madaraja kuanzia Elfu hamsini,laki moja,milioni moja na milioni tatu,na huwezi amini tiketi sold out kitambo,imagine.
Katika mahojiano hayo Zari alieleza kuwa amefurahi kuonana na mtu kama Diamond,kijana anaejiamini,anaejituma na ni msanii anaefanya kazi zake kwa kujituma na juhudi kubwa,mwenye upendo na mapenzi ya kweli kutoka moyoni,alisema Zari huku akitoa tabasamu laini na kuongeza kuwa hajutii kumpata Diamond katika maisha yake.
Kwa upande wake Diamond nae alikiri wazi kumpenda Zari katika nyanja zote,amesema kwa sasa amekuwa na furaha kila wakati, kwa kuwa hivi karibuni anatarajia kupata mtoto wa kike kutoka kwa mchumba wake Zari.
Mtangazaji wa Clouds 360 Hudson Kamoga akimuuliza swali Bi.Zari ambae ni Mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki na kwingineko.
Diamond akirekebisha jambo kwa mpenzi wake
Ooh..relax baby.
Ooh Shemejiiii......karibu..karibu Clouds FM/Clouds TV...! Mtangazaji wa Clouds FM kupitia kipindi cha Power breakfast,Gerald Hando akimkaribisha Zari The Bosslady kabla ya kuanza mahojiano ya moja kwa moja kupitia Clouds FM na Clouds TV.
All this, while the majority of Tanzanians still live beyond the poverty line. Chonde chonde Mola atunusuru, kwani walala hoi hawa ipo siku watafunua macho na kusema, "enough is enough". Patakuwa hapakaliki hapo kwani watataka pia WAGAWIWE haki yao, just me thinking.
ReplyDeleteHata diamond pia alikuwa mlalahoi. Ila kuwa mjasiri ndio kumemuinua. Na nyie mfanye kazi kwa bidii.
ReplyDeleteYour thinking is very negative. Tipical Tanzanian wivu mwingi no kusifia.
ReplyDeleteYaani hapo ndiyo utafahamu vichwa vya watanzania wengi vilivyo, mtu hafanyi kazi halafu anataka awe na pesa wapi na wapi. Huyo dogo anajituma sana sasa watu watataka na wao wagawiwe nini sasa. Kelele zile zile za mara oooh! watu mafisadi sawa mafisadi wapo lakini wewe umefanya jitihada zipi kuhakikisha unajitoa katika umaskini??? Fanyeni kazi baza acheni uvivu. Mtaendelea kusubiri sana siku ya huo mgao na haifiki wakati wenzenu wanakata mawimbi
ReplyDelete